Zantel yatoa msaada wa shilingi milioni kumi kwa ajili ya kukarabati madarasa sita ya shule ya Msingi Mkanyageni iliyoko Pemba.

August 19, 2015

2
Mkuu wa Shule ya Msingi Mkanyageni, Bwana Ramadhani Ngwali Makame, akitoa neno la utangulizi wakati wa makabidhiano ya hundi ya shilingi milioni 10 baina ya shule hiyo na kampuni ya Zantel kanda ya Zanzibar. Makabidhiano hayo yamefanyika leo shuleni hapo.
3
Mkurugenzi wa Biashara wa kampuni ya Zantel upande wa Zanzibar, Bwana Mohamed Musa akikabidhi hundi ya Shilingi millioni 10 kwa Mwenyekiti wa Shule ya Msingi Mkanyageni, Bwana Ally Ngwali Vuai iliyoko visiwani Pemba kwa ajili ya kukamiIsha ujenzi wa vyumba sita vya madarasa vitakavyotumiwa na watoto zaidi ya 350. Anayeshuhudia ni Mkurugugenzi wa Mauzo Zantel, Bwana Sukhwinder Bajwa pamoja na wanafunzi na wajumbe wa kamati ya shule hiyo.
………………………………………………………
Na Mwandishi wetu
Kampuni ya simu za mkononi ya Zantel leo imetoa msaada wa shilingi milioni 10 kama mchango wa kujenga madarasa sita katika shule ya msingi ya Mkanyageni iliyopo Pemba.
Kiasi hicho cha fedha kitatumika katika kumalizia ujenzi wa madarasa hayo sita kwa kuweka sakafu, madirisha na milango, kupaka rangi pamoja na gharama za kazi kiujumla, msaada ambao unatarajiwa kuboresha kiwango cha elimu katika shule hiyo.
Akikabidhi msaada huo, Mkurugenzi wa Mauzo wa kampuni ya Zantel,Bw Sukhwinder Bajwa alisema msaada huo umelenga kuboresha mazingira ya kusomea ya wanafunzi wa shule hiyo.
‘Kampuni ya Zantel mara zote imekuwa msitari wa mbele katika kuchangia kujenga nchi kwa kushiriki katika kuwekeza katika shughuli za kijamii hasa katika sekta ya elimu ambayo inaandaa mazingira na maisha bora ya viongozi wajao katika upatikanaji wa elimu’ alisema Bwana Bajwa.
Akizungumza pia wakati wa makabidhiano hayo, Mkurungezi wa Biashara wa Zantel upande wa Zanzibar, Mohamed Mussa alisema Zantel imejikita zaidi katika kuhakikisha watoto wanapata elimu bora visiwani hapa.
‘Kama kampuni inayoongoza kwa idadi kubwa ya wateja visiwani hapa ni wajibu wetu kuhakikisha tunajitolea kwa kuwekeza katika miradi inayogusa maisha ya wananchi kama huu wa elimu ambao unaboresha miundombinu ili watoto wetu waweze kupata elimu bora’ alisema Mussa.
Akitoa shukurani kwa kampuni ya Zantel kwa msaada, Mwenyekiti wa kamati ya shule, Bwana Ali Ngwali Vuai, alisema ni muhimu kuwekeza katika elimu kwani wanafunzi wakielimishwa watakuwa sehemu muhimu ya maendeleo ya taifa letu.
‘Tunawashukuru kampuni ya Zantel kwa kutusaidia katika juhudi zetu kuhakikisha tunaboresha mazingira ya elimu kwa watoto wetu’ alisema Bwana Vuai.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »