WAFANYAKAZI WA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI WAHAMASISHWA KUPIMA AFYA

August 19, 2015

 Daktari Hafidh Ameir toka Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS) akitoa elimu juu ya umuhimu wa kupima afya kwa wafanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi katika Semina iliyofanyika Makao Makuu ya Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
   Mfanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Marcelina Henry akichukuliwa vipimo vya shinikizo la damu na Muuguzi toka Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam, Asma Msimbe wakati wa zoezi la kupima afya kwa wafanyakazi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
   Bwana Ponela John wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi akichukuliwa vipimo vya urefu na Bwana John Joseph wa Timu ya Wataalamu waliofika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa ajili ya kupima afya za wafanyakazi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Mfanyakazi wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Bi. Radhia Said akichukuliwa vipimo vya urefu na Bwana John Joseph wa Timu ya Wataalamu waliofika Wizara hapo kwa ajili ya kuendesha zoezi la kupima afya za wafanyakazi wa Wizara hiyo jijini Dar es Salaam.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »