RADIO 5 YAMKABIDHI MFUGAJI BORA KANDA YA KASKAZINI PIKIPIKI KUMWEZESHA KUFIKIA MALENGO

August 18, 2015

Meneja Masoko wa Radio 5 ,Sarah Keiya akizungumza kwenye kikao kabla ya kumkabidhi mshindi wa kwanza zawadi ya Pikipiki yenye thamani ya sh. milioni 2 mfugaji bora Kanda ya Kaskazini,John Alfayo ambaye ni mkazi Kijiji cha Olmotony wilaya ya Arumeru mkoa wa Arusha.

Meneja wa Benki ya Akiba Commercial tawi la Arusha(ACB)Issa Hango akizungumza namna mfugaji John Alfayo alivyonufaika na mikopo kutoka benki hiyo ambayo imemfanya kufikia mafanikio makubwa.

Meneja Masoko wa Radio 5 ,Sarah Keiya(kushoto) akipongezana na Meneja wa Benki ya Akiba Commercial tawi la Arusha(ACB)Issa Hango baada ya makabidhiano yaliyofanyika katika ofisi za Taso,Njiro jijini Arusha,wanaoshuhudia ni Bwana na Bi John Alfayo. 

Meneja wa Benki ya Akiba Commercial tawi la Arusha(ACB)Issa Hango (kulia)akimkabidhi Pikipiki mshindi wa kwanza katika ufugaji bora Kanda ya Kaskazini,John Alfayo na mkewe Hilda leo,anayeshuhudia ni Mwenyekiti wa Chama cha Wakulima Kanda ya Kaskazini,Arthur Kitonga.

Meneja Masoko wa Radio 5 ,Sarah Keiya(kushoto) akiwakabidhi John Alfayo na mkewe hati za Pikipiki iliyotolewa na kampuni hiyo ambayo imekua ikiwasaidia wakulima kukabiliana na changamoto mbalimbali.

Maafisa wa Chama cha Wakulima Kanda ya Kaskazini(Taso)wafanyakazi wa Benki ya ACB tawi la Arusha,Radio 5 ,watumishi wa halmashauri ya Arusha DC na mshindi wa ufugaji bora wakiwa katika picha ya pamoja baada ya makabidhiano.
Habari Picha na Filbert Rweyemamu-Arusha

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »