Katibu Tawala Mkoa wa Lindi awaaga wasaidizi wake Baada ya Kuchaguliwa kugombea Ubunge CCM Jimbo la Nanyamba Mtwara

August 15, 2015

unnamed
Katibu Tawala Mkoa Mkoa wa Lindi,Abdallah Dadi Chikota ambae hivi Karibuni Alichaguliwa na Wana CCM kuwania nafasi ya Ubunge Jimbo la Nanyamba  Mtwara na Kupitishwa na Kamati kuu na Halmashauri kuu ya CCM Kuwania Jimbo Hilo akiwaaga wakuu wa Idara na Vitengo katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa.
unnamedm
Wakuu wa Idara na Vitego Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi wakiwa katika Kikao kazi Ambapo Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi alitumia Fursa kuagana na wasaidizi wake.
…………………………………………………
Na ABDULAZIZ ,Lindi
Wafanyakazi wa Sekriterieti ya Mkoa wa Lindi wametakiwa Kudumisha mshikamano na Ushirikiano katika Utekelezaji wa Miradi Mbalimbali ya Maendeleo Inayotekelezwa na ikiwemo mchakato wa  Ujenzi wa Wodi ya Kisasa na Nyumba ya Ghorofa kwa Madaktari wa Hospital ya Mkoa wa Lindi Ujenzi unaotarajiwa Kuanza
Wito huo Umetolewa Jana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Lindi,Abdallah Dadi Chikota alipokuwa akiwaaga Wakuu wa Idara Na Vitengo Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi kufuatia Kushinda Katika Kura za Maoni na Kuteuliwa na Chama Cha Mapinduzi kuwania Ubunge katika Jimbo la Nanyamba Mkoani Mtwara
Uteuzi wa CCM NA Baadae kuteuliwa na Tume ya Uchaguzi itamfanya Katibu Tawala huyo Kukoma Rasmi Ajira  ya Utumishi wa Umma Serikalini kwa Mujibu wa Taratibu za Kiutumishi
Akiongea na Wakuu hao,Chikota ambae katika Uongozi wake Alifanikiwa Kuunganisha Watumishi wake kufuatia Uwepo wa Makundi aliyoyakuta kutokana Na Mgogoro Uliokuwepo kutokana Migongano ya Kiutendaji iliyokuwepo katika Sekriterieti Hiyo
Aidha Chikota aliwataka Watumishi wa Serikali Kumpa Ushirikiano Mkubwa Bw Grayson Mwaigombe ambae atakakuwa Akikaimu Nafasi Hiyo anayoicha ambapo alisisitiza Kufanya kazi kwa kufuata Mifumo ya Ufuatiliaji na Usimamizi wa Miradi na Fedha Miradi kutumika kama ilivyooanishwa katika Bajeti ya Serikali
‘Watumishi wenzangu Nawashukuru sana kwa Ushirikiano Mlionipa kwa kipindi chote nilichokuwa nanyi Naomba Kuwasisitiza ni lazima ili kufikia mafanikio lazima Muwe na Vikao vya Mara kwa Mara kupeana Mrejesho na Muhimu kuzingatia Fedha za Miradi zitumike kwa kufuata Utaratibu na Miongozo Iliopo kwa Manufaa ya UMMA na isiwe kwa Ajili Binafsi  ‘Aliwasihi Chikota
Katika Uongozi wake miradi aliyoicha katika Utekelezaji ni Pamoja na Nyumba ya Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kilwa,Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Ruangwa,Nyumba za maofisa Tarafa pamoja na Ujenzi wa Wodi ya Kisasa na Nyumba ya Ghorofa kwa ajili Ya Madaktari wa Hospital ya Mkoa wa Lindi na Ukarabati wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa
Nae Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Lindi,Grayson Mwaigombe kwa Upande wake alieleza kuwa ataendeleza Mipango Yote Iliyoachwa na Chikota kwa kukamilisha Miradi ambayo Imeanza na Ile ambayo Imepangwa Inasubiri Pesa Toka Hazina Huku akizitaka Halmashauri zote Kutekeleza agizo la Serikali la Kutumia Asilimia 60 YA Mapato ya Ndani kwa Miradi ya Maendeleo kusaidia utoaji wa Huduma za Jamii Ikiwemo Ujenzi wa Maabara,Vyumba Vyumba vya Madarasa,Numba za Waganga na Zahanati na Vituo Vya Afya Katika Mkoa huo
Chikota kabla ya Kuteuliwa kuwa Katibu Tawala Mkoa wa Lindi alipitia Nyadhifa Mbalimbali Ikiwemo Afisa Elimu wilaya,Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Newala Hivi karibuni katika Mchakato wa  Kutafuta Mgombea Ubunge Aliomba Ridhaa hiyo ambayo alishinda kwa Kishindo katika Uchaguzi wa CCM Jimbo la Nanyamba na Kupitishwa na Kamati kuu na Halmashauri Kuu ya CCM kuwania Nafasi hiyo katika Uchaguzi Mkuu Ujao

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »