ABDULRAHMAN KINANA AMPA MWAKYEMBE MWEZI MMOJA KUTOA MAJIBU

December 01, 2014

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa mjini Mtwara katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye  viwanja vya Mashujaa mjini humo akihitimisha ziara yake ya siku 16 aliyoifanya katika mikoa ya Lindi na Mtwara akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2010 inayotekelezwa na serikali kwa kushirikiana na wananchi wenyewe na kuhimiza uhai wa chama cha Mapinduzi CCM, Katika ziara hiyo Katibu mkuu huyo aliongozana na Nape Nnauye Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi, Katika kutano huo Kinana amempa wiki mbili Waziri wa Uchukuzi Dr. Harrison Mwakyembe kutoa maelezo kwanini bidhaa mbalimbali hazisafirishwi kwenda nje
kupitia bandari ya Mtwara, Lakini pia Kinana amewaagiza Waziri wa Nishati na Madini kutoa maelezo ni kwanini wawekezaji wenye kampuni zinazofanya shughuli zao mtwara wanalipia kodi zao jijini Dar es salaam badala ya kulipia mkoani Mtwara ambako wanafanya shughuli zao, Pia waziri wa Ofisi ya Mkamu wa Rais Mazingira amepewa mwezi mmoja kuhakikisha dampo la taka za sumu zinazotupwa na wachimbaji wa gesi na viwanda kuacha mara moja kwa sababu zinahatarisha maisha ya wakazi wa Mtwara, Mwisho akaagiza Ofisi ya Waziri Mkuu kutoa kibali cha kugawa viwanja katika manispaa ya Mtwara kwani viwanja vimeshapimwa, Fedha za kulipa fidia zipo ila kibali kutoka ofisi ya Waziri mkuu ndiyo kimkwama kwa muda wa mwaka mmoja sasa.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA FULLSHANGWE-MTWARA)

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »