April 01, 2014

Kesi dhidi ya Rais Kenyatta yaahirishwa


Rais Uhuru Kenyatta
Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC imehairisha kesi dhidi ya rais wa Kenya Uhuru Kenyatta hadi tarehe saba Oktoba mwaka huu.
 Rais Kenyatta anatuhumiwa kwa makosa ya jinai kufuatia machafuko ya baada ya uchaguzi wa mkwaka 2007 - 2008, madai ambayo ameyakanusha.
Hii ni mojawapo ya sababu kuu ya kubadili tarehe ya kusikizwa kwa kesi hii.
Upande wa mashitaka umesema kuwa unaipa Kenya muda wa ziada ili kutafuta na kuwasilisha baadhi ya stakabadhi za benki zinazohitajika katika kesi hiyo.
Kumekuwa na malalamishi kutoka kwa upande wa mashitaka kuwa serikali ya Kenya inalenga kuzuia stakabadhi hizo kufikishwa mahakamani jambo ambalo mawakili wa bwana Kenyatta wamekanusha.
Miongoni mwa yale yanayohitajika kotini ni pamoja na taarifa ya maelezo ya fedha anazomiliki bwana Kenyatta.
Kesi hii imekumbwa na matatizo ya mashahidi kujiondoa na shutuma za mahakama hii kuonea viongozi wa bara Afrika.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »