April 01, 2014
SERIKALI ITAHAMISHA NA KUWONDOKA WANANCHI WAISHIO KANDO KANDO YA BONDE LA MTO MKOMAZI-JK

NA OSCAR ASSENGA,KOROGWE

SERIKALI imesema itahamisha makaburi na itawaondoa wananchi wote  wanaoishi kando kando ya bonde la mto mkomazi kwa kuwalipa fidia za makazi na mimea yao ili kupisha ujenzi wa  bwawa kwa ajili kuinua na  kuendeleza  kilimo cha umwagiliaji.




Rai hiyo ilitolewa hivi karibuni na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Dokta Jakaya Mrisho Kikwete  wakati akiwahutubia wananchi katika mkutano wa hadhara  uliofanyika katika viwanja vya mamlaka ya mji wa mombo wakati wa ziara yake ya kukagua shughuli za maendeleo ya wananchi wilayani korogwe.


Rais Kikwete  aliyasema hayo mara  baada ya   mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Korogwe Lucas Mweri kueleza kwamba  serikali ilishatoa kiasi cha shilingi milioni 800 ili kutengeneza mradi huo lakini wananchi walikataa kuondoka katika maeneo hayo kwa madai kwamba  ni maeneo yao ya siku nyingi kwa shughuli za kilimo, mifugo, makazi lakini pia  katika maeneo  hayo yapo makaburi ya ndugu zao.


Rais kikwete  aliwaeleza wananchi kuwa  hakuna  mwananchi mwenye ardhi , Ardhi ni ya serikali na kwamba mwenye mamlaka ya mwisho  katika ardhi ni Rais hivyo amesema wananchi hao wataondolewa katika maeneo hayo kwa hali yoyote na gharama yoyote na kwamba hakuna kaburi lolote litakalo tumbukia katika  bwawa hilo.



Kikwete alisema makaburi yote  yatatafutiwa  maeneo maalum kwa kuhamishwa  mabaki ya miili na kuzikwa upya  kwa imani za kidini za ndugu zao.


Hata hivyo alisema serikali inapotaka kufanya  jambo lolote la maendeleo hakuna kikwazo kitakachowekwa na mwananchi yeyote, na kwamba ni lazima serikali iendelee kuelekeza nguvu zake katika kilimo ili wananchi waweze kujikwamua na umaskini.

Rais alisema  bonde hilo ni miongoni mwa maeneo yanayoonekana kuwa mkombozi wa maisha ya watanzania hivyo serikali itapeleka nguvu katika eneo hilo ili kuendeleza kilimo cha umwagiliaji na uhifadhi wa mazingira.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »