MSANII D.DOCTOR AKIWA KATIKA POZI LEO |
MSANII nguli wa mziki wa
Bongofleva mkoani Tanga, Dominick Mndeme “D.Doctor amejitokeza hadharani na
kukanusha habari zilizokuwa zimeenezwa kuwa amefariki dunia kwa kusema sio
kweli.
Akipiga stori na TANGA RAHA BLOG,D.Doctor alihabarisha kuwa
habari hizo zilivumishwa Desemba 29 mwaka jana na mmoja kati ya wasanii nguli
wa jijini Tanga ambaye ni rafiki yake wa karibu kitendo ambacho kilimshangaza
sana.
“Mimi sijafa ni mtu tu alichukua simu yangu bila
mimi kujua akaanza kueneza habari kuwa mimi nimekufa na aliweza kufanya hivyio
baada ya mimi kuzidiwa kilevi na kuzima ghafa ndio jamaa huyo nisiyemjua ndipo
alipoamua kueneza habari hizo hali ambayo iliwafanya marafiki na ndugu zangu
kushtuka sana na kudhani habari hizo ni za kweli “Alisema D.Doctor.
MSANII WA MZIKI WA BONGOFLEVA MKOANI TANGA,DOMINICK MNDEME "D.DOCTOR"AKIWA KATIKA PICHA |
Alisema baada ya kutokea
hali hiyo aliweza kupokea simu kutoka
nchi mbalimbali ambao walikuwa na lengo la kuthibitisha habari hizo ambao
walikuja kubaini kuwa habari hizo hazina ukweli wowote.
Aidha aliwaomba radhi
mashabiki wake,ndugu na marafiki zake kwa usumbufu wowote ambao ulijitokeza na
kuwataka mashabiki wake watarajie kupata ngoma kali ambazo zinakuja hivi
karibuni.