MKUU WA MKOA WA RUKWA AONANA NA WATAFITI KUTOKA TAASISI YA UTAFITI WA KILIMO UYOLE MBEYA KUJADILI KUINUA KILIMO CHA NGANO MKOANI RUKWA

May 15, 2014

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza na watafiti kutoka taasisi ya Utafiti wa Kilimo Uyole iliyopo Mkoani Mbeya walipomtembelea ofisini kwake leo kutambulisha mpango wa SARD (Strategic Agriculture Reseach Development) unaodhaminiwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika ADB (Africa Development Bank). Mpango huo una lengo la kupunguza utegemezi wa chakula nchini kwa kuongeza uzalishaji wa vyakula mbalimbali ikiwemo zao la ngano ambalo ni sehemu ya mradi huo Mkoani Rukwa.
Katika kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alisisitiza juu upatikanaji wa masoko ya kudumu kwa mazao yatakayozalishwa katika mpango huo badala ya kuwekeza nguvu katika uzalishaji pekee.
Ndugu Anthony Elanga mtafiti kutoka Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Uyole Jijini Mbeya ambae pia ni Mratibu wa Utafiti wa Zao la Ngano Tanzania akizungumza katika kikao hicho. Amesema mpango huo utahusisha wakulima na vikundi vya wakulima ambao watapatiwa elimu na kuwezeshwa mikopo mbalimbali ya kuendeleza kilimo cha ngano Mkoani Rukwa.
Mkutano ukiwa unaendelea.
(Na Hamza Temba – Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @rukwareview.blogspot.com)

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »