March 04, 2014

*VITA KALI YA MASAA MATANO CHATU NA MAMBA, MAMBA HOI ATOLEWA MAJINI NA KUMEZWA

Nyoka aina ya Chatu akipambana na Mamba ndani ya maji.
Nyoka huyo baadaye alifanikiwa kumzidi nguvu Mamba na kumuua na kisha kumtoa ndani ya maji hadi nchi kavu na kuanza kummeza.
******************************************
Katika hali isiyokuwa ya kawaida na isiyotarajiwa na wengi, Nyoka mkubwa aina ya Chatu ameibuka na ushindi kwa kumsinda nguvu Mamba akiwa ndani ya maji na kisha kumtoa nchi kavu na kummeza, huko Kaskazini mwa mji wa Queens Land.

Tukio hilo lililotokea juzi lilivuta hisia za watu wengi walioshuhudia vita hiyo,  katika ziwa Moondarra lililopo karibu na mlima Isa, ambapo baadhi ya walioshuhudia tukio hilo walivutiwa na vita hiyo na kuanza kunasa tukio hilo katika kamera zao.

Imeelezwa kuwa nyoka huyo aliyekuwa na urefu wa Futi 10,  alijipinda na kujiviliga kwenye mwili wa Mamba na kupambana naye na kisha kumtoa majini na kuanza kummeza, ambapo Chatu huyo alitumia dakika 15 kumla Mamba huyo hadi kummeza baada ya mpambano wao uliochukua kiasi cha masaa matano, huku wote wakionekana kuchoka.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »