TAARIFA KWA VYOMBO VYA
HABARI
Machi 4, 2014
TFF KUWACHUKULIA HATUA ZAIDI WAWILI TWIGA STARS
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linatafakari hatua
zaidi za kinidhamu dhidi ya wachezaji wawili wa kikosi cha Twiga Stars
walioondolewa kwenye timu hiyo na Kocha Rogasian Kaijage.
Kocha Kaijage aliwatimua kambini wachezaji Mwapewa Mtumwa na Flora
Kayanda kutokana na vitendo vya utovu wa nidhamu wakati Twiga Stars ikijiandaa
kwa mechi ya marudiano ya michuano ya Afrika kwa Wanawake (AWC) dhidi ya
Zambia.
Twiga Stars ilipoteza mechi ya kwanza ugenini mabao 2-1 na kutoka
sare ya bao 1-1 katika mechi ya marudiano iliyochezwa Februari 28 mwaka huu
Uwanja wa Azam Complex, hivyo kutolewa katika mashindano hayo kwa jumla ya
mabao 3-2.
TFF tunaunga mkono hatua iliyochukuliwa na Kocha Kaijage dhidi ya
wachezaji hao wakongwe wa Twiga Stars, kwani katika shughuli yoyote ile
inayohitaji ufanisi nidhamu ni kitu cha kwanza.
Twiga Stars itacheza mechi za mchujo za michezo ya 11 ya Afrika
(All Africa Games) ambayo itafanyika mwakani nchini Congo Brazzaville.
Boniface
Wambura Mgoyo
Media
and Communications Officer
Tanzania
Football Federation (TFF)