"Kamati
ya PAC imemaliza kikao chake na Wizara ya Ardhi, Fungu 48. Wizara
imetekeleza agizo la Kamati la kutoa upya hati za umiliki wa Ardhi
ambapo kumbukumbu za ardhi zitaunganishwa na mfumo wa namba za mlipa
kodi na vitambulisho vya Taifa. Hati salama zisizogushika (ngumu
kugushi). Kamati imeridhia mchakato uendelee ili kuanza kazi hiyo kwa
awamu na kwa kuanzia na mkoa wa Dar Es Salaam."
|