LIVERPOOL
kwa mara ya kwanza ndani ya miaka mitano iliyopita wamepata ushindi
katika dimba la Old Trafford baada ya kuwafumua wenyeji Manchester
United mabao 3-0.
Nahodha
mashuhuri wa Liverpool na timu ya Taifa ya Uingereza, `Mr. Liverpool`,
Steven Gerrard alifunga mabao mawaili, huku bao la tatu likitiwa
kambani na Luis Saurez.
Gerrard
alifunga kwa penati dakika ya 34 baada ya Rafael kuushika mpira kwa
mkono, na alifunga penati nyinginie dakika ya 46 kufuatia Phil Jones
kumfanyia madhambi Joe Allen eneo la hatari.
Nyota
huyo wa England angefunga mabao matatu `Hat-Trick` katika dimba la Old
Trafford tangu mwaka 1936 endapo angefanikiwa kutia kambani penati ya
tatu waliyopewa dakika ya 79 baada ya Nemanja Vidic kumfanyia
madhambi Daniel Sturridge, lakini alikosa penati hiyo.
Vidic
alitolewa nje kwa kadi nyekundu, lakini penati ya tatu inaonekana
haikuwa halali kwani Sturridge alionekana katika video akimdanganya
mwamuzi na kushinda janja yake.
Kikosi
cha Man Utd leo: De Gea 6, Rafael 5,Jones 5, Vidic 5, Evra 5.5,
Fellaini 5 (Cleverley 76, 6), Carrick 5, Mata 4.5 (Ferdinand 87),
Rooney 4.5, Januzaj 5 (Welbeck 76, 6), Van Persie 4.5.
Kikosi
cha Liverpool: Mignolet 7, Johnson 7, Skrtel 8, Agger 7.5, Flanagan
7.5, Henderson 7.5, Gerrard 8.5 (Lucas 87), Allen 8, Sterling 6
(Coutinho 72, 6), Sturridge 8, (Aspas 90+1), Suarez 8.
Pengo kubwa: Liverpool sasa wapo mbele kwa pointi 14 dhidi ya Man United na pointi 4 nyuma ya vinara Chelsea.
Amewazamisha kwao: Suarez akifunga bao lake katika mchezo wa leo
Tofauti: Suarez akiwapa dole wenzake kwa kazi nzuri, wakati huo huo Wayne Rooney anawalaumu wenzake
Kwa pamoja: Wachezaji wa Liverpool wakishangilia ushindi wao
Aibu kubwa: United wapo nyuma kwa pointi 14 dhidi ya Liverpool, ambao sasa wanaonekana washindani wa ubingwa msimu huu