Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akisaini kitabu cha maombolezo ya msiba wa Lefoord Simba, mtoto wa Waziri wa Maendeleo
ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, wakati alipofika nyumbani kwa Waziri
Masaki jijini Dar es Salaam, leo kutoa pole.
Marehemu Lefoord Simba, enzi za uhai wake.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akimfariji
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, wakati alipofika
nyumbani kwake Masaki jijini Dar es
Salaam, leo kutoa pole kwa kufiwa na mtoto wake, Lefoord Simba. Mazishi
yatafanyika kesho kwenye Makaburi ya Kinondoni.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza
na Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, wakati alipofika
nyumbani kwa Waziri Masaki jijini Dar es Salaam, leo kutoa pole kwa kufiwa na
mtoto wake, Lefoord Simba. Mazishi yatafanyika kesho kwenye Makaburi ya
Kinondoni.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akijumuika na Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamini Mkapa, Waziri mstaafu
(wa pili kulia) Mjumbe wa Nec Wilaya ya Busega, Chegeni (kulia) na Mwenyekiti
wa CCM Mkoa wa Shinyanga, Khamis Mgeja, wakizungumza jambo wakati wakijumuika
kwa pamoja katika maombolezo ya msiba wa Lefoord Simba, mtoto wa Maendeleo ya
Jamii, Jinsia na Watoto, Sophia Simba, Masaki jijini Dar es Salaam, leo.
Baadhi ya waombolezaji......