WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Innocent Bashungwa
WAZIRI
wa Nchi, Ofisi ya Rais- TAMISEMI, Innocent Bashungwa amesikia kilio
cha Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina aliyehoji sababu ya Serikali
kutozifungua Zahanati 10 zilizojengwa na kukamilika kwa miaka mingi sasa
huku wananchi wa vijiji hivyo wakilazimika kutembea umbali mrefu
kutafuta huduma.
Akichangia bajeti ya Wizara ya Afya bungeni
Dodoma Mei,2022, Mpina alisema upungufu wa watumishi wa kada ya Afya
ngazi ya Zahanati ni tatizo ambalo halijapata suluhu kwa muda mrefu na
wananchi wakiendelea kukosa huduma hitajika katika vijiji vingi vya
Jimbo la Kisesa.
Mpina alisema Serikali ilipaswa kuweka
utaratibu mzuri wa ajira na kutumia njia mbadala ya kuingia 4 mkataba na
vijana waliohitimu mafunzo mbalimbali ya Afya ambao hawaja ajiriwa ili
kusaidia utoaji wa huduma kwa wananchi.
“Mheshimiwa Spika,
Kwenye Jimbo langu la Kisesa nina Zahanati 10 zilizokamilika muda mrefu
lakini huduma hazitolewi, Mfano Zahanati ya Kijiji cha Semu, Mwandu
Kisesa, Makomangwa, Mwageni, Mwagayi, Isangijo, Ikigijo, Mwakisandu,
Malwilo na Tindabuligi, lakini pia tuna maboma ya muda mrefu 10 ya
Kijiji cha Inonelwa, Mwamhongo, Nzanza, Matale, Masanga, Mwakipugila,
Ntobo, Ng’hanga, Mwakasumbi na Lubiga” alisema Mpina.
Hata hivyo
kwa mujibu wa orodha ya majina ya watumishi wapya wa sekta ya Afya
iliyotangazwa na Waziri Bashungwa Juni 26, 2022 kwa Jimbo la Kisesa
zitafunguliwa Zanahati 6 kati ya 10 zilizokamilika ujenzi wake.
Waziri
Bashungwa amezitaja Zahanati hizo mpya zilitakazofunguliwa rasmi kwa
Jimbo la Kisesa na idadi ya watumishi wapya kwenye mabano kuwa ni
Zahanati ya Kijiji cha Isangijo Kata ya Lubiga (3), Zahanati ya Kijiji
cha Makomangwa Kata ya Mwandoya (3), Zahanati ya Kijiji cha Mwagayi Kata
ya Itinje (3).
Pia Waziri Bashungwa amezitaja zahanati nyingine
zitakazofunguliwa Jimbo la Kisesa kuwa ni Zahanati ya Mwageni Kata ya
Isengwa (3), Zahanati ya Kijiji cha Mwasungura Mwageni B (2), Zahanati
ya Kijiji cha Malwilo Mnadani Kata ya Tindabuligi (3), Zahanati ya
Mwandu Kisesa Kata ya Kisesa (3).
Waziri Bashungwa amewataja
watumishi hao na majina ya vituo vyao kwenye mabano kuwa kuwa ni Teodora
Kalistus Chodota Muuguzi Daraja la II, Ayubu Gladwell Mwaibosi Muuguzi
Daraja la II na Ramadhani Shabani Mrutu, Tabibu Daraja la II (Co)
(Zahanati ya Isangijo).
Wengine ni Joseph Rashid Ghake, Muuguzi
Daraja la II, Edomu Anania Mwakingwe, Muuguzi Daraja La II, Frank John
Mandala Tabibu Daraja la II (Zahanati ya Makomangwa).
Bashungwa
amewataja wengine kuwa ni Nuru Daud Mwala , Muuguzi Daraja la II na
Ernest Joseph Kachwele, Muuguzi Daraja la II (Zahanati ya Malwilo).
Wengine ni Samwel Gelewa Simon, Muuguzi Daraja la II, Maryam Baraka
Omar Female, Tabibu Daraja la II (CO) na Yohana Magori Magori, Muuguzi
Daraja la II (Zahanati ya Mwagayi).
Wengine ni Azizi Poul
Mgoboleni, Tabibu Daraja La II (Co), Johnson Joseph Kayombo, Muuguzi
Daraja la II na Damian Emanuel Lyimo, Muuguzi Daraja la II (Zahanati ya
Mwageni). Bertha Juvenary Nyamwiula, Muuguzi Daraja la II na Nkeshimana
Jumanne Kasonga, Muuguzi Daraja la II (Zahanati ya Mwageni B-
Mwasungura).
Wengine ni Kissile Nelson Mwakabago, Muuguzi Daraja
la II, Eufransia Zacharia Mjuanga, Muuguzi Daraja la II na Ezekiel
Christopher Mantyotyo, Tabibu Daraja la II (Co) (Zahanati ya Mwalilo
Mnadani). Watumishi wengine ni Thereza Revocatus Lweyemaho, Muuguzi
Daraja la II, Kasilda Gervas Nkembo, Tabibu Daraja la II (CO) (Zahanati
ya Mwandu Kisesa).
RAIS SAMIA AZINDUA MIF,AIPONGEZA KWA KAZI NZURI KWA WATOTO WA KIKE
Na John Mapepele
WADAU WAPONGEZA MIF KWA KUSAIDIA MTOTO WA KIKE ZANZIBAR, WAJITOKEZA KUCHANGIA
WAZIRI MCHENGERWA AIPONGEZA TIMU YA KRIKETI KUTWAA UBINGWA RWANDA, AMSHUKURU RAIS SAMIA
UWEKEZAJI MKUBWA KUFANYWA NA SERIKALI KATIKA SEKTA YA KILIMO CHA UMWAGILIAJI– MNDOLWA
Mkurugenzi
Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Raymond Mndolwa akiongea na
waandishi wa Habari baada ya mkutano na watumishi wa Tume ya Taifa ya
Umwagiliaji na wahandisi wa Umwagiliaji wa Mikoa, uliofanyika Jijini
Dodoma mapema leo.
Mkurugenzi
Mkuu Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Raymond Mndolwa na Baadhi ya
watumishi wa Tume hiyo pamoja na wahandisi wa Umwagiliaji wa mikoa
Baadhi ya watumishi wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakifuatilia kikao kilichofanyika jijini Dodoma mapema leo.
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw, Raymond Mndolwa amesema, kutakuwa na kilimo cha umwagiliaji cha uhakika kutokana na uwekezaji mkubwa wakihistoria unaofanywa na serikali ya awamu ya sita katika sekta ya kilimo cha umwagiliaji.
Bw,Mndolwa ameyasema hayo mbele ya Waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari jijini Dodoma mara baada ya kufungua kikao kazi kilichowahusisha watumishi wote wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na kuongeza kuwa, kutokana na majukumu makubwa iliyopewa na serikali Tume ya Taifa ya Umwagiliaji “niliona ni muhimu sana tukutane watumishi wote ili tujipange,tuweze kutekeleza majukumu hayo”.
“Tume tuna juku la kuwasaidia wakulima waweze kulima kutokana na kilimo wanacholima ili waweze kupata maji katika mazao wanayolima hili ni sehemu ya majukumu yetu, kutokana na hali yakuwa na upungufu wa mvua serikali imeweka msisitizo mkubwa katika kilimo cha umwagiliaji kwa matarajio yajayo”.
Tunataka Wananchi na Wakulima waliokata tamaa ya kulima warudi shambani, kwasababu tume ya Taifa ya Umwagiliaji imewezeshwa na inakuja kufanya mageuzi makubwa katika sekta ya kilimo cha Umwagiliaji.
Akizungumzia suala la Bajeti kubwa iliyoelekezwa na Serikali ya awamu ya sita katika Sekta ya Kilimo cha Umwagiliaji, Mkurugenzi Mndolwa ameongeza kusema kuwa, Tume imeelekeza nguvu katika miradi iliyokwisha buniwa na miradi hiyo ndiyo ya kipaumbele, baada ya miradi hiyo ya mwaka huu hatua itakayofuata ni kujenga miradi mingine ya umwagiliaji nchini katika maana ya mikoa yote itakayotekeleza kilimo cha umwagiliaji na aina gani ya miradi ifanyike katika kuhakikisha kila Mkoa na Wilaya inapata miradi ya Kilimo cha Umwagiliaji.
Alisema wana panga upya kuhakikisha kwamba mwaka wa fedha unaofuata yaani 23/24 watakuwa na mkakati ambao utaenea nchinzima.
Mwaka wa fedha huu 22/23 watarekebisha Skimu thelathini (30) za kilimo cha umwagiliaji lakini Wahandisi wa umwagiliaji wa mikoa watafanya mapitio ya miradi iliyokwisha kwa lengo la maboresho kulinga na na bajeti yetu.
“Nina ahidi kwamba maboresho yatakuwa makubwa ili kila mwananchi anayetaka kulima aweze kulima.”Alisisita Kikao cha leo ni majumuisho ya siku yapili ya kikao kilichohusisha watumishiwa Tume Makao makuu na Wahandisi wa Umwagiliaji wa mikoa kilichojadili, Mpango mkakati wa miaka mitano wa utekelezaji wa shughuli zaTume.
TANZANIA NA INDIA KUJA NA MAPINDUZI MAKUBWA KWENYE UTAMADUNI
SOUTHAMPTON KUWANOA MAKOCHA WA TANZANIA -WAZIRI MCHENGERWA
MNDOLWA AONGOZA MAPITIO YA MPANGO MKAKATI WA MIAKA MITANO WA TUME YA TAIFAYA UMWAGILIAJI
MkurugenziMkuu, Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Raymond Mndolwa akifungua kikao kazi cha mapitio ya mpango mkakati wa miaka mitano wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Jijini Dodoma.
Mhandisi wa Umwagiliaji wa Mkoa wa Singida William Kadinda akielezea namna mpango mkakati utakavyorahisisha utekelezaji kiutendaji katika maeneo husika.
Baadhi ya Wataalam wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakijadiliana kwa lengo la kuboresha Mpango Mkakati wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji.
Picha ya pamoja kati ya Menejimenti ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Wahandisi wa Umwagiliaji wa Mikoa.
Na; MwandishiWetu - Dodoma
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw. Raymond Mndolwa, ameongoza kikao kazi cha mapitio ya mpango mkakati wa miaka mitano wa Tume ya Taifa ya umwagiliaji, uliohusisha wataalam na wahandisi wa Umwagiliaji nchini, mapema leo Jijini Dodoma.
Bw. Mndolwa alisema kuwa,kuna umuhimu wakufanya mapitio ya mpango mkakati huo kwa pamoja tofauti kwa kuwa Mpango mkakati huo ni Dira ya Taasisi hivyo ni muhimu kila mtumishi katika taasisi anatakiwa kuifahamu kwani ndiyo zana inayotumika katika utekelezaji wa kazi za kila siku.
“Nimeona kuna Umuhimu wa kupitia kwa pamoja ili pale ambapo patakuwa na marekebisho turekebishe kwa pamoja, na kuwe na ushiriki kwa hoja katika kazi hii.” AlifafanuaMndolwa.
Kwa upande wake Mhandisi wa Umwagiliaji wa Mkoa wa Singida William Kadinda amesema, kikao kazi hiki kinatoa fursa ya mpango wa miaka mitano ambao unajumuisha shughuli zinazofanyika, pia kinaangalia maslahi ya watumishi katika upande wa mafunzo na kuona mahitaji yao, nakuweza kuwaongezea uwezo kiutendaji.
Kukamilika kwa mpango mkakati huo ni hatua muhimu kwa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji wakati huu,ikiwa na jukumu kubwa la ukarabati na ujenzi wa Skimu za umwagiliaji pamoja na Mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji. Lengola serikalini kufikia Hekta 1,200,000 za umwagiliaji mwaka 2025.
KIONGOZI WA MABOHORA DUNIANI ATUA NCHINI KUFANYA ROYAL TOUR TANZANIA
TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI KUJENGA MABWAWA 14 NA HEKTA ELFU 10 ZA UMWAGILIAJI KWAAJILI YA UZALISHAJI WA MBEGU, SHILLINGI BILIONI 420 KUTUMIKA.
Mheshimiwa Hussein Bashe Waziri waKilimo akizungumza wakati akifungua semina ya siku mbili iliyowahusisha wadau wa Sekta ya Umwagiliaji mjini Morogoro
Mheshimiwa Hussein Bashe Waziri waKilimo akizungumza wakati akifungua semina ya siku mbili iliyowahusisha wadau wa Sekta ya Umwagiliaji mjini Morogoro
Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji,Bw, Raymond Mndolwa akizungumza wakati wa semina hiyo
Picha ya Pamoja ya Wajumbe mbalimbali walioudhuria Semina hiyo Walioketi. Katikati ni Waziri waKilimo Mheshimiwa Hussein Bashe.
NA MWANDISHI WETU,MOROGORO
Waziri wa
Kilimo Mheshimiwa Hussein Bashe, amesema kwa Mwaka wafedha ujao Wizara
yake itatumia Shilingi Bilioni 420 katika ujenzi wa Miundo mbinu ya
Skimu za umwagiliaji ikiwemo Hekta elfu kumi kwa ajili ya uzalishaji wa
Mbegu ambapo wadau wa sekta binafsi watapewa kipaumbele kwa ajili ya
kuzalisha Mbegu, ujenzi wa mabwawa 14 yatakayokuwa na miundombinu ya
umwagiliaji kwa matumizi ya kilimo na mifugo.
Eneo lingine la kipaumbele kwa Waziri Bashe ni pamoja na kuwasaidia Wakulima Wadogowadogo kupataTeknolojia bora za kilimo cha umwagiliaji kwa bei nafuu ili waweze kupata tija na kuchangia ongezeko la mavuno katika sekta ya umwagiliaji, zoezi hilo litawahusu pia Vijana wanaojishughulisha na kilimo cha umwagiliaji.
Kwaupande wake Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Bw,Raymond Mndolwa amewataka watumishi wote wa tume ya Taifa ya Umwagiliaji kufanya kazi kwa bidi na ubunifu ili kutimiza matarajio yaliyowekwa na serikali, akiamini taasisi yake inauwezo wakutekeleza majukumu yaliyopangwa na serikali kwa wakati, ufanisi na ubora unaotakiwa katika kuhudumia wananchi.
“ Nitamsapoti kila mtumishi aweze kutimi za wajibu wake, tumejipanga na lililopo mbele yetu tunaweza kulitekeleza”
Semina hiyo ya siku mbili imewashirikisha wadau mbalimbali ikiwemo sekta binafsi, Wakulima wadogo, Wataalam waBenki, Vyama vya Ushirika, Wahandisi na Maafisa kilimo wa Wilaya ikiangazia namna ya kuboresha maeneo matatu muhimu katika kilimo cha umwagiliaji ,uzalishaji, huduma za u mwagiliaji na njia bora yakukusanya Ada naTozozaUmwagiliaji.
MTUME BONIFACE MWAMPOSA AFIKA NYUMBANI KWA MBUNGE WA KISESA, LUHAGA MPINA KUHANI MSIBA MAMA YAKE NA KUMBUKUMBU YA MZEE MPINA
Mtume Boniface Mwamposa Bulldoza akiendesha maombi kwenye Kaburi la Mama yake mzazi Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina, Marehemu Kephrine Kabula Masaga aliyezikwa Juni 8, 2022 pamoja na kumuombea Baba Mzazi wa Mpina Marehemu Mzee Mpina Gabisi Samweli Luchemba Hafla hii imefanyika Kijiji cha Isangijo Wilaya ya Meatu Mkoa wa Simiyu Juni 15, 2022.