Na John Mapepele
Waziri
 wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa pongezi 
kwa  Timu ya Tanzania ya  Wanawake ya Kriketi kwa  kutwaa Ubingwa leo 
Juni 18, 2022 kwenye mashindano ya Kwibuka Cup nchini Rwanda, 
yaliyoshirikisha nchi nane ( Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Botswana , 
Nigeria, Brazil na Ujerumani) bila kufungwa na timu yoyote. 
Aidha, amempongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwa mchango wake mkubwa anaoutoa katika michezo.
Amesema
 hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuboresha michezo kwa kuweka 
mikakati  kabambe chini ya uongozi wa Samia imeleta matokeo chanya 
kwenye sekta za michezo na sanaa hapa nchini.
Amesema
 taarifa ya hali ya uchumi wa nchi iliyosomwa bungeni hivi karibuni 
imeonesha kuwa sanaa na burudani zimechangia kwa asilimia 19.4 katika 
kipindi cha mwaka 2021 na kuziacha kwa  mbali sekta mbalimbali.
Amesema
 dhamira ya Serikali kwa sasa ni kuifanya michezo kuwa uchumi badala 
mazoe ya kuifanya michezo kama  kitu cha burudani pekee.
Aidha,
 amesema Serikali tayari inazigharimia timu zote za taifa zinazojiandaa 
kwa ajili ya mashindano ya kimataifa kwa kuziweka kambini kuanzia mwanzo
 wa mwaka huu.
Hivi 
karibuni Mhe. Mchengerwa amekaririwa vyombo vya habari akisisitiza kuwa 
michezo na sanaa ni uchumi  hivyo wanamichezo na wasanii wanapaswa 
kutambua kuwa vipaji walivyonavyo ni mtaji wa maisha yao.
Ujumbe
 wa Klabu ya Southampton uliokutana na Mhe. Waziri Mchengerwa na kufanya
 mazungumzo ya kuinua michezo ulioongozwa na Mkuu wa Idara ya Biashara 
ya klabu hiyo David Thomas pia ulimpongeza Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan
 kwa kazi kubwa anayoifanya kwenye michezo na kumzawadia jezi ambayo 
ilipokelewa kwa niaba yake na Mhe. Mchengerwa.
 



 
EmoticonEmoticon