Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(kulia)
akiteta jambo na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe.Amos Makala wakati wa
ufunguzi wa mafunzo ya wataalaamu wa Wakala wa Barabara mijini na
Vijijini(TARURA) yaliyofanyika Jijini Mbeya.
Mkurugenzi wa barabara Vijijini
Mhandisi Abdul R.Digaga akitoa taaarifa ya awali kwa mgeni rasmi
kuhusiana na mafunzo ya masuala ya Ununuzi wa Umma na Usimamizi wa
Mikataba ya Ujenzi na matengenezo ya barabara na Maadili katika kazi za
TARURA yaliyofunguliwa leo Jijini Mbeya.
Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo akizungumza
na wahandishi, wajumbe wa bodi ya zabuni na wataalamu wengine wa TARURA
wa mikoa saba ya Nyanda za juu kusini wakati wa mafunzo ya Ununuzi na
maadili yanayofanyika Jijini Mbeya.
Baadhi ya wataalamu wa TARURA
wakifuatilia hotuba ya Waziri wa Nchi,OR-TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo
wakati akifungua mafunzo ya Manunuzi na Maadili Jijini Mbeya.
Katika Picha ya pamoja ni ni
Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI Mhe.Selemani Jafo(Aliyekaa katikati) pamoja
na viongozi wa Mkoa pamoja na TARURA na washiriki wa mafunzo kutoka Mkoa
wa Njomba.
Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo(kushoto)
akiteta jambo na Mkurugenzi wa barabara Vijijini Mhandisi Abdul R.Digaga
baada ya ufungzuzi wa mafunzo ya TARURA jijini Mbeya.
………………
Nteghenjwa Hosseah, Mbeya
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amewataka
watumishi wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijiji(Tarura) kuvunja
utatu usio mtakatifu katika kazi za ujenzi na matengenezo ya barabara
zinazoendelea kutangazwa katika maeneo mbalimbali Nchini.
Waziri Jafo ameyasema hayo
wakati wa kufungua mafunzo ya Siku Sita ya watalaam wa Tarura kutoka
katika Mikoa saba ya Nyanda za Juu kusini kuhusiana na masuala ya
Ununuzi wa Umma na Usimamizi wa Mikataba ya Ujenzi na matengenezo ya
barabara na Maadili katika kazi za TARURA yenye takribani miezi sita
sasa tangu kuanzishwa kwake.
Waziri Jafo amesema
“Ninaposema Utatu mtakatifu namaanisha Afisa Manunuzi, Mhasibu na
Mhandishi wa Tarura katika eneo husika hawa ndio huwa wanaamua nani
apewe kandarasi kwa mujibu wa mahusiano na makubaliano wanayoyajua wao.
” Huu Utatu usio mtakatifu
katika kazi za Umma ufe kuanzia leo na Mkandarasi apewe kazi kwa
kuzingatia uwezo wake wa kitaalam na kifedha katika kukamilisha kazi
hiyo na sio mahusiano na makubaliano nje ya vigezo vilivyowekwa”.
Katika Utatu huu
ninauouzungumzia kuna mahusiano ya karibu sana na Rushwa na inafahamika
wazi kuwa Rushwa hupofusha wataaalam kuona na kutathmini uwezo wa
Mzabuni, huzorotesha kazi iliyopangwa kufanyika na kuwanyima wananchi
haki yao ya Msingi ya huduma bora za barabara na tutakaowabaini
wakiendeleza kasumba hii tutawachukulia hatua za kisheria na kinidhamu
alisema Jafo.
Akimkaribisha Waziri wa Nchi
Ofisi ya Rais, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Amos Makala amesema
wamejiandaa kikamilifu kusimamia kazi za Tarura na baada ya uzinduzi wa
kitaifa walizindua tena Kimkoa ili kuwafahamisha wananchi wa Mkoa huu
umuhimu wa Taasisi hii, ili waweze kumiliki Kazi zinazofanywa na Tarura
na kuwaeleweshe lengo la kutoka kazi za barabara kutoka Halmashauri na
kusimamiwa na Tarura.
“Tarura imekuja kuboresha kazi
nzuri iliyokuwa ikifanywa na Baraza la Madiwani, Kamati za kudumu
pamoja na Ofisi ya Mkurugenzi sasa TARURA wamekuja kutekeleza kitaalam
zaidi, namna ya usimamizi, manunuzi, mikataba ili tuweze kupata matokea
bora na ya haraka.
Naye Mkurugenzi wa Tarura Eng.
Abdul R. Digaga amesema Mafunzo haya ni mpango wa Kimakakati wa
Tarura katika kupambana na Rushwa katika utekelezaji wa miradi ya Ujenzi
na matengenezo ya barabara, mgongano wa maslahi, matumizi mabaya ya
fedha zilizotengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara na ukosefu wa
Uadilifu miongoni mwa watendaji.
Mafunzo hayo ambayo yalianza
kufanyika katika kanda mbalimbali Nchini na kanda hii ya Nyanda za juu
kusini ni ya mwisho kufanyika kwa wataalam wa Tarura wa kada mbalimbali
na imejumuisha Mikoa ya Mbeya, Songwe, Ruvuma,Rukwa,Katavi na Iringa na
Njombe.