Mshauri
elekezi wa mradi wa upanuzi na ujenzi katika Chuo Cha Uuguzi Mtwara NTC
na Chuo Cha Maafisa Tabibu Mtwara CoTc Arch. Benjamini Kasiga aliyevaa
fulana ya bluu akiwakilisha mada katika kikao kifupi kilichofanyika
chuoni hapo wakati wa ukaguzi wa majengo ya chuo hiko uliofanywa na jopo
la Wakaguzi kutoka Wizara ya Afya Mkoani Mtwara.
Mkandarasi
kutoka kampuni ya Ujenzi na Uhandisiz Nandhra wa kwanza kushoto akiwapa
maelezo baadi ya wakaguzi wa jengo hilo kutoka Wizara ya Afya wakati wa
ukaguzi wa majengo ya Chuo Cha Uuguzi Mtwara na Chuo Cha Maafisa Tabibu
Mtwara CoTc uliofanyika leo mkoani humo.
aimu
Mkurugenzi wa kitengo cha kusanifu Majengo Wizara ya Afya Arch. Daniel
Mwakasungura aliyevaa shati jekundu akiangalia moja ya sehemu ya jengo
la Chuo Cha Uuguzi Mtwara NTC na Chuo Cha Maafisa Tabibu Mtwara CoTc
wakati wa ukaguzi wa majengo ya chuo hiko uliofanyika leo mkoani humo,
katikati ni Mratibu wa ujenzi huo Dkt. Joachim Catherine na kulia ni
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ununuzi na Ugavi Wizara ya Afya Bw. Castro
Simba.
engo
la wagonjwa Kutoka nje la Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini ambalo
lipo kwenye ujenzi bado ambapo limegharimu kiasi cha shilingi Bilioni 1.
7 za Kitanzania na lengo la ujenzi wa Hospitali hiyoni kuweza kutoa
huduma za kibingwa.Picha Na Wizara ya Afya-MTWARA
Baadhi
ya Majengo ya Chuo Cha Uuguzi Mtwara NTC Chuo Cha Maafisa Tabibu Mtwara
na CoTc yakiwa yamekamilika katika mradi wa ujenzi wa Ujenzi,Upanuzi na
ukarabati wa majengo ya chuo hiko na Chuo Cha maafisa Tabibu mtwara
yalipokaguliwa na wakaguzi wa jengo hilo kutoka Wizara ya Afya leo
mkoani Humo.
NA WAMJW-MTWARA
SERIKALI
Kupitia Wizara ya Afya imeagiza Kampuni ya Ujenzi na Uhandisi Nadhra
kumalizia kazi ya kurekebisha kasoro zilizotokana na ujenzi katika
majengo ya Chuo Cha Uuguzi Mtwara ( NTC) na Chuo cha Maafisa Tabibu
mkoani humo (COTC) ili kuweza kudahili wanafunzi wengi zaidi.
Hayo
yamesemwa na Mkurugenzi wa Ununuzi na Ugavi Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bw. Castro Simba wakati wa ukaguzi wa
majengo hayo mkoani Mtwara.
“Majengo
haya yalimalizika Desemba 2016 tukatoa kipindi cha mwaka mmoja
kujiridhisha na ubora wake lakini kuna baadhi ya maeneo hayajakidhi
ubora hivyo mkandarasi anatakiwa kurekebisha ndani ya mwezi mmoja”
alisema Bw. Simba.
Aidha
Bw. Simba amesema kuwa mradi huo wa kupanua, kukarabati na kujenga
majengo hayo yanafanyika katika vyuo vitano nchini ikiwemo Hospitali ya
Kairuki Dar es salaam, Bagamoyo, Chuo cha Uuguzi Mtwara (NTC), Chuo Cha
Maafisa Tabibu (CoTC) na Chuo cha St. Bakhita cha Sumbawanga.
Kwa
upande wake Mratibu wa Kuimarisha Mifumo ya Afya na Mratibu wa Mradi huo
kutoka Wizara ya Afya Dkt. Joachim Catherine amesema kuwa mradi huo
uliofadhiliwa na Global Fund umehusisha ujenzi Wa mabweni matatu yenye
vyumba 120, Nyumba za watumishi nane katika chuo cha maafisa tabibu.
Katika na Chuo cha uuguzi Mtwara.
Aidha
Dkt. Catherine amesema kuwa Miradi yote imegharimu kiasi cha Shilingi
bilioni 3.3 za kitanzania na kulifanyika ukarabati na upanuzi Wa
madarasa, ofisi za wakufunzi, maktaba pamoja na maabara za vitendo.
Kwa
upande wake Mkuu wa Chuo Cha Uuguzi Mtwara (NTC) Bw. Frolian Mbungu
amesema kuwa amefurahishwa na ukaguzi huo kwani utamfanya apokee majengo
kwa kujiamini na kuyatumia kwa ufasaha.
Aidha
wakaguzi hao kutoka Wizara ya Afya wakiongozwa na Mkurugenzi wa Sera na
Mipango Dkt. Edward Mbanga walitembelea jengo la wagonjwa Kutoka nje la
Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kusini ambalo limegharimu kiasi cha
shilingi Bilioni 1. 7 za Kitanzania na lengo la ujenzi wa Hospitali hiyo
ni kuweza kutoa huduma za kibingwa.