KATA YA KISESA YAKUMBANA NA CHANGAMOTO ZA KIMAZINGIRA

May 02, 2016



Aliyeshika kipaza sauti ( kushoto), Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akizungumza na wakazi wa kijiji cha Mwabukoli kilichopo katika kata ya Kisesa wilayani Meatu, wakati wa Ngoma ya Mavuno maarufu kwa jina la kabila la wasukuma Mpuhumulo wakati wa ziara yake ya utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kupanda miti na kuhifadhi vyanzo vya maji, Mkoani Simiyu.

Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Mwabukoli wilayani Meatu Mkoani Simiyu, wakifuatilia Hotuba ya Naibu Waziri Mpina (hayupo Pichani) alipotembelea kijijini hapo, wenyeji hao wa kabila la kisukuma, wapo na vifaa vyao vya jadi wakifanya dawa kwa utaratibu wa kudumisha mila zao wakati wa ngoma ya mavuno.    
Sehemu wa Wakazi wa Kijiji cha Mwabukoli, wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri Mpina (Hayupo Pichani) alipokuwa akiwafafanulia namna ya kukabiliana na changamoto za utunzaji wa mazingira katika ziara yake Mkoani Simiyu ya Utekelezaji wa mkakati wa kitaifa wa kupanda miti na kuhifadhi vyanzo vya maji.

Pichani Naibu Waziri Mpina akikaa katika Chanja akiwa ameshikilia mkuki..ni ishara ya utemi kwa kabila la kisukuma, wakati wa ngoma ya mavuno kijijini Mwabukoli, kabla Hajaongea na wananchi wa kijiji hicho kuhusu kukabiliana na changamoto kubwa waliyonayo ya kuhifadhi mazingira na vyanzo vya maji.
                     EVELYN MKOKOI,MEATU


Wakazi wa kijiji cha Mwabukoli kilichopo Wilayani Meatu Mkoani Siiyu katika kata ya Kisesa, wamekumbana na Changamoto za kimazingira kutokana na kile kinachodaiwa ni utekelezaji wa sheria ya mazingira ya mwaka 2004 kifungu 57 (1)  kinachokataza shughuli zozote za kibinadamu  ndani ya mita sitini (60) ya vyanzo vya maji, mito, maziwa na bahari.
Sheria hiyo ya  mazingira imewabana wakazi wa kata ya Kisesa, Mwabawa,Mwasegela na Lingeka kutokana na kuwakataza wananchi wa kata hizo wasifanye shughuli zozote za kibinadamu kama vile kufanya kilimo, kuchota maji, kuchunga na kulisha mifugo, kuchota mchanga, kukusanya kokoto, kuchimba  na kuponda mawe.
Katazo hilo la serikali linatoakana na sababu kuwa maeneo hayo yana ardhi oevu na yenye rutuba na kutokana na hali ya ukame katika maeneo ya mkoa huyo ardhi hii inaruhu mazao kustawi vizuzi.
Awali akitolea ufafanunuzi wa suala zima la uhifadhi wa mazingira na vyanzo vya maji, waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Raisi Muungano na Mazingira mhe. Luhaga Mpina alisema kuwa, serkali ya Tanzania ilipata ufadhili kutoka  Mfuko wa mazingira wa dunia dunia (GEF), Bank ya Dunia na shirika la (SIDA) kupitia mradi wa Program ya kuhifadhi mazingira wa ziwa Victoria ( LVEMP )
 Naibu Waziri Mpina, alieleza kuwa   awamu ya kwanza ya mradi huo uliokuwa ukisimamiwa  na Ofisi ya Makamu wa Raisi kupitia  Baraza la Taifa la Hifadhi na Usumamizi wa Mazingira (NEMC),  uliojulikana kama mradi wa kuhifadhi ziwa Victoria, (LVEMP) uliwataka wananchi kuibua miradi mbadala itakayo wawezesha wananchi kufanya shunguli mbadala za kiuchumi bila kuharibu mazingira, kama vile ufugaji nyuki, bustani, ufugaji kuku, samaki na kilimo cha matrekata wangombe wa kisasa.
Mhe. Mpina aliwafafanulia wakazi wa kata hizo katika mkutano wake wa hadhara ulofanyika kijijini Mwabukoli kuwa, awamu ya pili ya mradi huo unahusisha nchi za afrika mashariki, ambapo hapa nchini kwa sasa suala hilo lipo chini ya wizara ya maji lakini atachukua jukumu la kuongea na wizara na sector husika ili kuona ni namana gani wananchi wanaweza kunufaika na mradi huo.
Aidha, akiwasilisha changamoto hizo diwani wa kata ya kisesa (CCM) mhe. Sasa Kishola alieza kuwa pamoja na miradi hiyo mbadala kuibuliwa bado haijatoshelesha mahitaji  ya wananchi  kiuchumi, hivyo kupitia mkakati huu wa kitaifa wa kupanda miti na kuhifadhi vyanzo vya maji, serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Raisi iangalie namna ambavyo wakazi wa kata hizo watakavyoweza kutumia maeno hayo uoevu kupanda miti ya biashara kama vile miti ya matunda na miti ya mbao ili kuweza kuinua kipato chao na kukuza uchumi wa nchi bila kuharibu mazngira.
 Ziara hiyo ya Naibu WAziri Mpina Wilayani Meatu mwishoni mwa wiki, ilikuwa na lengo la kushiriki usafi wa mazingira pamoja na utekelezaji wa mkakati wa kitaifa ya kupanda miti na kuhifadhi vyanzo vya maji.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »