Kamati ya Rufaa ya Nidhamu ya
Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kesho Jumanne Mei 3, 2016 saa 5:00
asubuhi itatangaza uamuzi wa rufaa nane zilizowasilishwa na kujadiliwa
za viongozi, mchezaji na timu tatu zilizoshiriki Ligi Daraja la Kwanza
Tanzania Bara 2015/2016.
Kamati hiyo itatangaza uamuzi
huo mbele ya waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Mikutano wa ofisi za
TFF, zilizoko kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es
Salaam.
Jumla ya rufaa nane zinazohusu
timu, kocha, viongozi na mchezaji mmoja zilijadilikuwa na kamati hiyo
kwa Jumapili Mei mosi, 2016 kwenye ofisi za TFF jijini.
Rufaa zilizojadiliwa kwenye kikao hicho ni za:
- Timu ya Geita Gold
- Choki Abeid ambaye ni Kocha Msaidizi wa timu ya soka ya Geita Gold FC
- Denis Richard Dioniz – Kipa wa Geita Gold
- Fatel Rhemtullah – Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Tabora
- Saleh Mang’ola – Mwamuzi wa Soka wa Mkoa wa Dodoma
- Timu ya Soka ya Polisi Tabora
- JKT Oljoro Fc ya Arusha
- Yusufu Kitumbo – Mwenyekiti wa Chama cha Soka Mkoa wa Tabora
Wadau hao wa soka walikata rufaa
dhidi ya uamuzi wa Kamati ya Nidhamu baada ya kamati hiyo kuwatia
hatiani na kuwaadhibu kwa makosa ya kupanga matokeo ya michuano ya Ligi
Daraja la Kwanza. Wakata rufaa wote walihudhuria kikao cha rufaa zao.