Kamanda wa polisi Mkoani Tanga akiwaonyesha waandishi wa habari mabegi na viroba vilivyajaa
mirungi na bangi vilivyokamatwa katika kizuizi cha polisi Kwamkwale Wilayani
Korogwe jana.
Kukamatwa kwa madawa hayo ni kutokana na jitihada za askari polisi kuzidisha ukaguzi katika vizuizi vyake ambapo
inadaiwa wasafirishaji wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali za usafirishaji
ikiwemo kuweka katika mabegi ya nguo na magunia ya mkaa, polisi wamekuwa katika
wakati mgunu wa kuweza kugundua.
Hata hivyo kamanda Poul amesema
mbinu zote wamezigundua hivyo kuwatahadharisha wasafirishaji wa madawa ya kulevya kuwa
wamezigundua na yoyote ambaye atagundulika atapalekwa Mahakamani moja kwa moja
wakati uchunguzi ukiendelea pamoja na kuwasaka vinara wa waagiziaji wa madawa
ya kulevya.