Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akishiriki kazi ya kuchimba mtaro
pamoja na viongozi wa mkoa wa Dodoma kwa ajili ya kufukia mabomba
katika mradi wa maji wa Kata ya Mundemu kijiji cha Nguji katika wilaya
ya Bahi wakati alipotembelea mradi huo na kukagua shughuli za ujenzi wa
tanki la maji na usambazaji wa mfumo wa mabomba akiwa katika ziara yake
ya kikazi mkoani Dodoma, Kinana yuko Katika ziara ya mikoa ya Dodoma,
Arusha na Kilimanjaro akikagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM
ya mwaka 2010 akiongozana na msemaji wa chama hicho Katibu wa NEC
Itikadi na Uenezi Bw. Nape Nnauye pamoja na viongozi mbalimbali wa chama
na serikali katika mkoa wa Domoma.(PICHA NA KIKOSIKAZI CHA
FULLSHANGWE-BAHI-DODOMA)
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wananchi wa kijiji cha Nguji kata ya Mundemu mara baada ya kukagua mradi huo na kushiriki katika shughuli za ujenzi.
Kutoka
kulia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dodoma Mh. Adam Kimbisa, Mh. Badwel
Mbunge wa jimbo la Bahi na Luteni Mstaafu Chiku Galawa Mkuu wa mkoa wa
Dodoma wakimsikiliza Ndugu Abdulrahman Kinana hayupo pichani wakati
alipokuwa akizungumza na wananchi katika kijiji cha Nguji.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikagua
mradi wa umeme wa jua ambao ni maalum kwa ajili ya kuendesha kisima cha
maji ya kumwagilia mashamba ya zabibu katika kijiji cha Lamaiti.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana
na wananchi mbalimbali wakati alipotembelea mradi shamba la zabibu
katika kijiji cha Lamaiti wilaya ya Bahi ili kujioneautekelezaji wake.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiongozana
na Mkuu wa mkoa wa Dodoma Luteni Mstaafu Chiku Galawa huku wakiwa
wameshika majembe tayari kwa kushiriki katika shughuli ya kusafisha
shamba la Zabibu katika kijiji cha Lamaiti.
Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na ujumbe wake wakiendelea na
shughuli za kusafisha shamba kwa ajili ya upandaji wa miche ya mizabibu
Lamaiti.
Moja
ya nyumba za walimu zinazojengwa katika kijiji cha Kongogo kata ya
Babayu ambayo katibu mkuu aliikagua na kushiriki katika ujenzi wake.
Mbunge wa jimbo la Bahi Mh. Badwel akizungumza na wananchi huku Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza katika kijiji cha Kongogo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akivishwa mgorole kama ishara ya kupewa heshima ya wazee wa kijiji cha Chonde.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipungiana mkono na wananchi mara baada ya kupewa heshima ya wazee wa kijiji cha Chonde kwa kumvisha mgorole.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizindua
mradi wa matrekta katika kijiji cha Chonde ambapo vikundi 12 vinamiliki
matrekta 19 yanayofanya kazi ya kilimo katika mashamba ya wanavikundi
na wananchi kwa ujumla.
Nape
Nnauye naye akiendesha moja ya matrekta mara baada ya kuzinduliwa rasmi
na Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana katika kijiji cha
Chonde.
Wananchi wakinyoosha mikono yao juu kuashiria kukubali hotuba ya Katibu
Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati alipokuwa akizungumza nao
katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Chonde.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwahutubia wananchi wa kijiji cha Chonde wilayani Bahi wakati alipofanya ziara yake katika wilaya hiyo.
Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokelewa
na mamia ya wananchi katika kijiji cha Chonde ambapo pia ameshiriki
katika shughuli ya ujenzi wa zahanati ya kijiji hicho.
Nape Nnauye akiwasili katika eneo la mkutano katika kijiji cha Chonde.