ZAIDI ya Abiria elfu mbili waliokuwa wanasafiri kutoka mkoani Kigoma kuelekea mikoani wamekwama jana kusafiri kwa saa tisa katika mkoani Dodoma hali iliopelekea abiria hao kuandamana hadi ofisi ya mkuu wa mkoa kutafuta msaada
Imedaiwa kuwa abiria hao ambao walikuwa wakielekea jijini Dar es Salaamu walitumia zaidi ya wiki mbili njia waliamua kuandama hadi ofisi ya mkuu wa mkoa wa Dodoma mara baada ya kufika kaituo cha mamala yarely mkoani hapa na kupta taarifa kuwa hawaweze kuendelena safari kutokana na miundombinu ya Treli
Wakizungumza kwa jazba mbele ya mkuuu wa mkoa wa Dodoma Dkt Rehema Nchimbi baadhi ya abairia walisema wameanza safari tangu Januari 2 mwaka huu lakini mpaka sasa hawajaweza kufikia jijini Dar es Saalamu na kila siku wanmekuwa wakidanganywa na uongozi wa shirika hili huku wakiendelea kuteseka njiani
Mmoja wa abiria hao Wilkira James alisema tangua walipoanza safai Januari 2mwaka huu wamekuwapata matatizo nia na hakuna masaada wowote ulewanaopata kutoka kwa shirika hili hali wakiendelea kuchelewa njia na baadahi yaabiria wanafamilia zaopamoja na wagonjwa
“Mkuu wa tafadhali sana sisi tlianza safari mwanzoni mwa mwezi wa januari lakini pale Kigoma tulishamaliza wki moja kusubiri usafiri jamboambalo limesababisha tuishia maisha magumu hata kuendelea hata kuuuza vifaa vitu ili tupate huduma ”
“Tena hao viongozi wa stesheni hawana huruma kabisa pamoja na wao kusababisha sisi kukwama katika vituo bado wamekuwa wakiendelea kutulipiza huduma ndogo ikiwemo kupata huma za haja kubwa na ndogo, hata kuoga” alisisitiza abiraia huyo
Nae Salehe Selemani alisema kuwa tangu walipoanza safari kutoka Kigoma wamelala katika porini la usinge, Manyoni kwa madai kuwa kichwa treni hiyo kiliharibika jambo ambalo wao hawakujali gharama ambazo wamekuwa wakitumia pindi wanapolala
Alisema katika safari hiyo , kuna watu warika zote na jinsia zote ambapo wanawake wenye watoto wamekuwa katika hatari zaidi kutokana n amahitaji ya watoto walinao ambapo wamewkuwa wakikosa huduma muhimu jambo ambalo linaweza kuleta madhara makubwa zaidi indapo halitachukuliwa hatua haraka
Kwa upande mkuu wa mkoa wa Dodoma, Dkt Rehema Nchimbi alikiri kuwepo kwa tatizo hilo ambalo limesabishwa na mvua zinazonyesha maeneo yamikoa ya jirani na kuleta mafuriko katika mkoa huo ambayo yamesababisha kuharibika kwa eneo la stesheni za reli kati za Gulwe na Godegode wilayani Mpwapwa ambazo zimefaa maji
Alisema tatizo hilo wameanza kulishughulikia na mpaka majira ya saa kumi na moja ya Januari 9 mwaka abiria hao watakuwa wamepata ufumbumbuzi wa tatizo hilo na kuweza kuendelea na safari yao
Hata hivyo aliutaka uongozi wa kampuni ya Reli Tanzania TRL kuhakikisha kuwa unawapa huduma zote muhimu bure abira hao ikiwemo fedha kwa ajili ya chakula kwa abiria wakati wakiendelea na ufumbuzi wa tatizo hilo
Nae msimamizi wa kituo cha treni cha Dodoma mhandisi John Mandagu alisema kutokana na tatizo hilo alishawasiliana na uongozi wa TRL makao makuu na kukubaliana kuwapata huduma muhimu abiria mpaka watakapoweza kusafikiri na kufika jijini Dar es salamu
Alisema kuwa mpaka sasa wameanza kukarabati eneo la Gulwe na Godegode ambazo zimefaa maji ili kuweza kuwapatiawasafiri huduma na kuweza kufika walipokuwa wakienda jijiji Dar kwa ajili ya shughuli zao za ujenzi wataifa
Tatizo la safari zalilianza tangu Januari 2 mwaka huu ambalo uongozi TRL uliotoa taarifa kupitia ofisi ya Uhusiano kwa niaba ya kaimu mkurugenzi mtendaji mhandisi Paschal Mafikiri ikidai kuwa usafiri wa treni kutokaKigoma kwenda Dar umeharishwa kutoka na uharibu wa miundombinu