Na Oscar Assenga,Tanga.
MSANII Mpya wa Muziki wa BongoFleva hapa nchini,Juma
Pondamali “Mensa”amesema mziki huo unalipa sana kuliko hapa mchezo wa mpira wa
miguu ila itatagemea na umahiri ulionao katika kutoa mashairi mazuri.
Akizungumza na Tanga Raha,Pondamali ambaye hivi sasa anatamba na
wimbo wake “Pesa baba yako nani”ambao ameirekodi kwenye studio za Suleshi
alisema ameamua kuingia kwenye mziki huo sio kwa kutania bali ni dhamiri yake
aliyekuwa nayo muda mrefu.
Pondamali alienda mbali zaidi na kueleza anamshukuru
mwenyezi mungu kwa kumjalia kipaji cha utunzi mzuri na uimbaji kitu ambacho
kitampa wakati mzuri wakati akiwa katika harakati zake za kuachia album lakini
akisema wakati huu amepanga kuachia single tu.
“Ninamshukuru
mwenyezi mungu amenijali kipaji kizuri cha utunzi na sio kama ninatania
nimedhamiri kweli kufanya mziki kwa sababu unalipa kuliko ilivyo soka na
unaweza kuuza single moja tu ukapata fedha nzuri “Alisema Mensa.
Aidha aliongeza kuwa licha ya kuimba mziki hatoweza kuiacha
kazi yake aliyokuwa nayo hivi sasa kwani anaiheshimu na kuithamini hivyo atafanya
mziki na kufundisha soka kwani kila kitu hapo kinawakati wake na muda.
Pondamali ambaye pia ni Kocha wa Makipa kwenye timu ya
Taifa ya Tanzania “Taifa Stars”na timu ya Coastal Union ya Tanga alisema
malengo yake makubwa ni kuhakisha anafanya vizuri kwa kutoa nyimbo mzuri ambazo
zitaweza kumpa mafanikio zaidi.
EmoticonEmoticon