Waziri Ummy Mwalimu azindua jengo la Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania

January 25, 2018
index
Kibaha. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,  Ummy Mwalimu amesema serikali inafanyia kazi mkakati mpya wa utoaji mikopo kwa wanafunzi wa kada ya afya wanaosoma katika ngazi ya cheti na astashahada.
Waziri Ummy ameyasema hayo jana wakati akizindua jengo la Baraza la Uuguzi na Ukunga Tanzania lililopo Halmashauri ya mji Kibaha, mkoani Pwani.
Alisema kundi hilo ni muhimu linalopaswa kuangaliwa kwa jicho la pili, kwani ndilo linalotoa huduma kwa ukubwa wake katika sekta ya afya.
“Nipo katika mazungumzo ya awali na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Joyce Ndalichako kuangalia ni namna gani tutaiwezesha tasnia hii ikue ili tupate watumishi wengi zaidi wenye viwango, maana mzazi ataweza kulipa ada litakapofikia suala la chakula na mengineyo inakuwa shida,” alisema.
Alisema watumishi wa ngazi za uuguzi na ukunga wenye ujuzi na weledi wa kutosha pekee wanachukia takribani asilimia afya 60 ya watumishi wote wa afya nchini.
“Shirika la Afya duniani (WHO)  linasema kuwa, zaidi ya asilimia 80 ya huduma zote za afya hutolewa na wauguzi na wakunga, hivyo mimi binafsi, Wizara yangu na Serikali kwa ujumla tunaendelea kutoa kipaumbele katika kuhakikisha huduma za uuguzi na ukunga nchini zinaimarika vya kutosha,” alisema.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »