Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (kulia) akifungua
kikao cha Wawakilishi wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori hai
kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni kuiomba
Wizara kusitisha zuio la kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara,
kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Dkt. Nebbo
Mwina ( Picha na Lusungu Helela-MNRT)
Mwenyekiti wa Chama cha wasafirishaji wanyamapori hai nje ya
nchi, Enock Balilemwa akizungumza kwenye kikao cha cha Wizara
ya Maliasili na Utalii na Wawakilishi wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori
hai kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni
kuiomba Wizara kusitisha zuio la kusafirisha wanyamapori hai nje ya
nchi kibiashara. ( Picha na Lusungu Helela-MNRT)
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Wanyamapori, Dkt. Nebbo Mwina
akizungumza kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii,
Japhet Hasunga kufungua kikao cha Wawakilishi wa Wafanyabiashara
ya Wanyamapori hai kilichofanyika jana mjini Dodoma, ikiwa lengo
la kikao hicho ni kuiomba Wizara kusitisha zuio la kusafirisha wanyamapori
hai nje ya nchi kibiashara. ( Picha na Lusungu Helela-MNRT)
Makamu Mwenyekiti wa Chama cha wasafirishaji wanyamapori hai
nje ya nchi, Fatuma Hamisi akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Maliasili
na Utalii, Japhet Hasunga (hayupo pichani) kwenye
kikao cha cha Wizara ya Maliasili na Utalii na Wawakilishi wa Wafanyabiashara
ya Wanyamapori hai kilichofanyika jana mjini Dodoma ikiwa lengo la
kikao hicho ni kuiomba Wizara kusitisha zuio la kusafirisha wanyamapori
hai nje ya nchi kibiashara. ( Picha na Lusungu Helela-MNRT
Baadhi ya Wawakilishi wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori
hai wakimsikiliza Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga
wakati wa kikao kilichofanyika jana mjini Dodoma kati ya Wizara na wadau
hao lengo likiwa ni kuiomba Wizara kusitisha zuio la kusafirisha
wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara. ( Picha na Lusungu Helela-MNRT)
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga na Wawakilishi
wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori hai kwenye kikao kilichofanyika
jana mjini Dodoma, ikiwa lengo la kikao hicho ni kuiomba Wizara kusitisha
zuio la kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara. ( Picha na Lusungu Helela-MNRT
Mjumbe wa Halmashauri wa TWEA, Paul Madinda ambaye pia ni mmiliki wa shamba la viumbe hai jijini Arusha, akizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga (hayupo pichani) jinsi alivyoathirika tangu zuio hilo la kusafirisha wanyamapori hai nje ya nchi lilipotelewa kwenye kikao cha cha Wizara ya Maliasili na Utalii na Wawakilishi wa Wafanyabiashara ya Wanyamapori hai kilichofanyika jana mjini Dodoma. ( Picha na Lusungu Helela-MNRT |
Chama cha wasafirishaji wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara
(TWEA) kimeiomba serikali isitishe zuio la kusafirisha nje
wanyamapori hao ili wanachama wake waweze kujikwamua na hali ngumu
ya maisha inayaowakabili.
Wakizungumza mbele ya Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Japhet
Hasunga kwenye kikao cha Wizara na wawakilishi wa
Wafanyabiashara hao waliiomba serikali isikilize kilio chao.
Kwa upande wake , Mwenyekiti wa Chama hicho, Enock Balilemwa alisema
baadhi ya wanachama wakiwemo walemavu waliokuwa wamechukua mikopo
benki wamefukuzwa kwenye nyumba zao baada ya kushindwa kufanya marejesho
ya mikopo hiyo kufuatia zuio la biashara hiyo.
Alieleza kuwa baadhi ya wanachama wake wamejikuta kwenye hali ngumu
ya kupoteza mali zao na kuingia kwenye mifarakano na wateja wao kwa
vile wafanyabiashara hao walichukua pesa toka kwa wateja kama
malipo ya awali hivyo wakati wa zoezi la kusimamisha biashara linafanyika
liliwakuta wafanyabiashara hao wameshachukua pesa za wateja wao kama
malipo ya awali.
Naye, Makamu Mwenyekiti wa TWEA, Fatuma Hamis alimweleza Naibu Waziri
kuwa zuio hilo lilifanywa ghafla mno bila kutoa muda kwa wafanyabiashara
hao ukizingatia kuwa walikuwa wakimiliki leseni halali walizokuwa wamezilipia
pesa bila kuzifanyia kazi ya kuwaingizia kipato.
Aidha,
alimweleza Naibu Waziri huyo kuwa zuio hilo limepelekea wafanyabiashara
hao kupoteza uaminifu kwa wateja wao na kuwaweka kwenye mazingira magumu
ya ushindani kibishara kwani biashara hiyo haifanywi na Tanzania pekee.
Wakati akijibu hoja za Wafanyabiashara hao, Naibu Waziri wa
Maliasili na Utalii, Japhet Hasunga amewahakikishia Chama cha
wasafirishaji wanyamapori hai nje ya nchi kibiashara (TWEA) ,kuyafanyia
kazi malalamiko yao kadri itakavyowezekana na kuja na kauli moja ya
serikali.
Amesema lengo la serikali la kuzuia usafirishaji wanyamapori hao lilikuja
baada ya wafanyabishara ambao sio waaminifu kukengeuka kwa kuanza kujihusisha
na ujangili pamoja na kusafirisha wanyamapori ambao hawamo kwenye orodha
ya vibali walivyopewa.
‘’Dhumuni la serikali la kusitisha biashara hii ilikuwa
ni njema tu baada ya kuona wajanja wachache wananufaika huku wanyonge
wakibaki watazamaji kwenye rasilimali zao’’ alisema Hasunga
Hata hivyo, Naibu Waziri Hasunga alisema lengo la serikali halikulenga
kuwakomoa bali ni kutaka kuweka mfumo mzuri utakaomsaidia kila
Mtanzania aone ananufaika na rasilimali za nchi yake.
‘’Nimewasikiliza kwa umakini wa hali ya juu lakini hata hivyo
Serikali ina utaratibu wake wa kutoa majibu, tupeni muda ili tukitoa
majibu kuhusu hoja zenu kuwe na jibu moja kwa kila mmoja wetu’’
alisema
Katika hatua nyingine, Hasunga aliwataka wafanyabishara hao wasisite
kuonana nae muda wowote ule kwa kumpigia simu au kwa kuonana
nae pindi wanapokuwa na jambo la kutaka kuzungumza nae kwa ajili ya
manufaa mapana ya Wizara na nchi kwa ujumla.
Naye, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya wanyamapori, Dkt. Nebbo Mwina
aliwahakikishia wafanyabiashara kufanyia kazi malalamiko yao kutokana
na hoja za msingi zilizowasilishwa na wafanyabiashara
hao.
‘’Nimesikia baadhi ya malalamiko yenu ambayo kwa nafasi yangu
niliyo nayo kwa kushirikiana na watumishi walio chini yangu nitayashughulikia’’
alisema.