Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasili kwenye ukumbi wa
zamani wa Baraza la Wawakilishi Kikwajuni tayari wa Uzinduzi wa Baraza
la Vijana Zanzibar akiongozana na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji, Wazee,
Vijana, Wanawake na Watoto Mhe. Maudline Cyrus Castico pamoja na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Zanzibar Ndugu
Khamis Rashid Kheri
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akizungumza na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na
Watoto Mhe. Maudline Cyrus Castico wakati wa hafla ya uzinduzi wa Baraza
la Vijana Zanzibar
Sehemu ya waliohudhuria uzinduzi wa baraza la vijana Zanzibar.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akihamasisha vijana wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Vijana Zanzibar
akiwa pamoja na Waziri wa Kazi,Uwezeshaji, Wazee, Vijana, Wanawake na
Watoto Mhe. Maudline Cyrus Castico na Mwenyekiti wa Baraza la Vijana
Zanzibar Ndugu
Khamis Rashid Kheri.
Khamis Rashid Kheri.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan
akihutubia wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Vijana uliofanyika kwenye
ukumbi wa Baraza la Wawakilishi la Zamani, Kikwajuni.
Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais
………………
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema kuwa jamii haina
budi kutambua kuwa vijana wana fursa kubwa katika kuleta maendeleo ya
nchi .
Makamu wa Rais aliyasema hayo leo
wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Vijana Zanzibar uliofanyika kwenye
ukumbi wa Baraza la Wawakilishi wa Zamani Kikwajuni.
Makamu wa Rais alisema kuwa Baraza
la Vijana Zanzibar ni Chombo au jukwaa litakalowavusha vijana kufikia
maendeleo wanayohitaji kiuchumi, kijamii, kisiasa na kufuatana na kasi
ya maendeleo ya sayansi na teknolojia Duniani.
“Ni imani yangu kuwa Baraza hili
litakuza mioyo yenu ili muweze kujituma, kujiendeleza na kuwa mstari wa
mbele katika kuunga mkono serikali yenu pamoja na kutetea na kuyalinda
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar na kuenzi fikra za Muasisi wa Serikali ya
Mapinduzi ya Zanzibar, Marehemu Mzee Abeid Amani Karume (Mungu
amrehemu)”
Makamu wa Rais aliendelea kusema
kuwa Uzinduzi wa Baraza la Vijana Zanzibar ni mwendelezo wa mawazo ya
Wana Mapinduzi ya kutaka kuweka hali za wananchi kuwa sawa (Bora), na
kujenga Taifa lenye Vijana Imara.
Makamu wa Rais alisisitiza kuwa ni
matarajio yake kuwa Baraza la Vijana Zanzibar litaendeshwa kwa misingi
ya demokrasia na sheria, kanuni na miongozo ya taasisi itakavyoelekeza.
Baraza hilo linalotokana na Sera
ya Maendeleo ya Vijana ya Mwaka 2005, sera hii ndio iliyopelekea
kupitishwa kwa sheria nambari 16/2016 iliyoanzisha Baraza hilo, hatua ya
utekelezaji wa Mkataba wa Vijana Afrika 2006 ambapo Jamhuri ya Muungano
imeridhia.
Makamu wa Rais aliwataka Vijana
kuwa mstari wa mbele katika kutunza amani ya nchi, kutoa ushauri pale
wakiwa na mawazo mbadala, kutengeneza mtandao na kuitumia mitandao kwa
manufaa ya kuwaleta pamoja na kukemea vitendo vyote vya udhalilishwaji
wa watoto na wanawake.
Mwisho; Makamu wa Rais aliwataka
vijana hao kuwa wamoja na kujenga hali ya kujitegemea na badala kuwa
tegemezi, watetezi wan chi, kuibua mawazo mapya ya maendeleo na
washiriki kwa kupaza sauti katika mambo yanayowahusu.