Tigo yazindua mbio za Kili Half Marathon 2018, kufanyika March 4.

October 26, 2017

Kaimu mkurugenzi wa Tigo kanda ya kaskazini, Henry Kinabo    akijitambulisha wakati wa kuzindua mbio za Kili Half Marathon kwa mwaka 2018, mgeni rasmi alikuwa ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dr Harrison Mwakyembe. 
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dr Harrison Mwakyembe akizungumza wakati wa uzinduzi wa mbio za Kili Marathon kwa mwaka 2018, uzinduzi huo umefanyika jana jijini Dar es Salaam ambapo kampuni ya simu za mkononi ya Tigo itadhamini mbio za kilomita 21 kwa jina la Tigo Kili Half Marathon.

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Dr Harrison Mwakyembe akikata utepe kuashiria uzinduzi wa mbio za Kili Marathon kwa mwaka 2018, uzinduzi huo umefanyika jana jijini Dar es Salaam, kulia kwake ni  Kaimu Mkurugenzi wa Tigo kanda ya kaskazini, Henry Kinabo ambao wamedhamini mbio za kilomita 21 ziitwazo Tigo Kili Half Marathon

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »