Waziri
wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla amewasili Makao makuu
ya Wilaya ya Ngorongoro na kisha kufanya mkutano maalum na Kamati ya
Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo ambapo kisha atazungukia kwenye maeneo
yenye migogoro.
Waziri
Dkt.Kigwangalla ametua uwanja mdogo wa Wasso uliopo eneo la Loliondo na
kisha kukutana na viongozi hao wa Ulinzi na Usalama wakiongozwa na Mkuu
wa Wilaya hiyo Mh. Rashid Mfaume Taka.
Dk
Kigwangalla baada ya kumaliza kikao hicho maalum na wakuu hao,
anatarajia kutembelea maeneo yenye migogoro ili kubaini kiini cha
mgogoro wa eneo hilo la pori tengefu la Loliondo.
Aidha,
pia anatarajia kuzungumza na wananchi wa maeneo hayo pamoja na kufanya
mkutano wa wazi ikiwemo kusikiliza kero kutoka kwa wananchi hao.
Waziri
Dkt.Kigwangalla yupo Mkoani Arusha kwa ziara ya sita ambapo awali
alianza kutembelea Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA)mjini Arusha, na
baadae Mamlaa ya Hifadhi ya Ngorongoro ambapo pia aliweza kukutana na
jamii ya wafugaji wanaoishi kwenye hifadhi ya Ngorongoro kwa namna ya
kitatua migogoro kati yao na wahifadhi wa Ngorongoro.
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akishuka kwenye ndege
wakati akiwasili Loliondo kufuatilia kwa kina mgogoro unaoendelea
Loliondo.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akiongozana na na viongozi wa Wilaya ya Ngorongoro
Waziri
wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na
viongozi wa Wilaya ya Ngorongoro kwenye uwanja wa ndege wakati
akiwasili Loliondo kufuatilia kwa kina mgogoro unaoendelea wilayani
humo.
Mkuu wa Wilaya hiyo Mh. Rashid Mfaume Taka akimwakilisha Waziri Dk.Kigwangalla katika mkutano huo wa Kamati ya Ulinzi na Usalama