Mwenyekiti wa makampuni ya Kama
Group , Gagan Gupta wakati wa hafla ilyofanywa na kampuni hiyo ya Kamal
Steel Ltd kiwandani hapo wakati wa utoaji wa msaada wa viungo
bandia, kwa watu wenye ulemavu 16, vyenye thamani ya zaidi ya sh.
milioni 80, hafla hiyo ya kukabidhi msaada huo imefanyika hivi karibuni
jijini Dar es salaam.(PICHA NA JOHN BUKUKU-FULLSHANGWE-DAR ES SALAAM)
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akishukuru kampuni hiyo kwa msaada ilioutoa kwa
watanzania hao wenye ulemavu wa miguu ambapo yeye ndiye aliyewakabidhi
kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa Kamal Steel, Sameer Gupta.
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akimvisha mguu wa bandia Bw. Siaga Raphael Kiboko
mara baada ya kukabidhiwa kutoka kampuni ya Kamal Steel ya jijini Dar es
salaam kushoto ni Mwenyekiti wa kampuni hiyo Bw. Gagan Gupta.
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akizungumza na Bw. Siaga Raphael Kiboko kabla ya
kumkabidhi msaada wake wa viungo bandia vya mguu.
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akiongozana na Bw. Gagan Gupta ambaye ni mwenyekiti
wa kampuni ya Kalam Steel tayari kwa ajili ya kukabidhi msaada huo.
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akifurahia jambo na Bw. Siaga Raphael Kiboko mara
baada ya kumvisha mguu wake huku Mwenyekiti wa kampuni ya Kamal Steel
Bw. Gagan Gupta pamoja na viongozi wengine wa kampuni hiyo
wakishuhudia.
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akiongozana na Bw. Joshua Mwamunyange mara baada ya
kumvisha mguu wakena kuanza kujaribu kutembea.
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akimbidhi Bi Fatuma mguu wake wa bandia ikiwa ni
msaada kutoka kampuni ya kutengeneza chuma ya Kamal Steel ya jijini Dar
es salaam.
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akiwa katika picha ya pamoja na wakuu wa kampuni ya
Kamal Steel na baadhi ya walemavu waliokabidhiwa msaada huo.
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk.
Harrison Mwakyembe akimsikiliza Mwenyekiti wa kampuni ya Kamal Steel
Bw. Gagan Gupta.mara baada ya kukabidhi misaada hiyo katikati
ni Mkurugenzi Mkuu wa Kamal Steel, Sameer Gupta na wakuu wengine wa
vitengo kutoka kampuni hiyo.
……………………………………………………………………………………………….
KAMPUNI ya kutengeneza chuma ya
Kamal Steel Ltd, imetoa msaada wa viungo bandia, kwa watu wenye ulemavu
16, vyenye thamani ya zaidi ya sh. milioni 80.
Akifunga kambi ya kutoa viungo
bandia hivyo jijini Dar es Salaam sambamba na kukabidhi vifaa hivyo,
Waziri wa Sheria na Katiba, Dk. Harrison Mwakyembe, alisema, serikali
itaendelea kuwawezesha watu wenye ulemavu nchini ili waweze kukabiliana
na changamoto zinazowazunguka ikiwa ni pamoja na kuwapatia vifaa
bandia.
Alisema, suala la ulemevu linagusa maisha ya kila mwanadamu na kwamba mtu yoyote anaweza kufikwa na tatizo hilo.
Alibainisha, viungo bandia
vinauzwa kwa ghalama kubwa ambayo watu wengi wenye ulemavu hawawezi
kumudu kununua hivyo serikali kwa kushirikiana na wadau wake
itaendelea kutoa msaada wa vifaa hivyo.
“Jamii iamini kuwa wote ni
walemavu watarajiwa. Kupoteza kiungo kimoja cha mwili ni changamoto
kubwa. Tunaishukuru kampuni ya Kamal Steel kwa kutoa misaada hii
muhimu ambayo tunaamini kuwa inasaidia kupunguza madhira ya
ulemavu,”alisema Dk. Mwakyembe ambaye kupitia msaada huo ameweza
kuwasaidia watu wenye ulemavu wanne kutoka jimbo lake la Kyela mkoani
Mbeya.
Mwenyekiti wa makampuni ya Kama
Group , Gagan Gupta, alisema,kampuni yake haijatoa viungo bandia hivyo
kama msaada, bali kama wajibu wake kwajamii.
“Tunaamini kwamba, viungo hivi
bandia vitawawezesha kumudu kutembea, kufanya kazi mbalimbali zitakazo
waletea kipato,”alisema Gupta.
Katika hatua nyingine, Gupta
aliahidi kumuajiri mmoja wawatu hao wenye ulemavu mwenye taaluma ya
ufundi mitambo, Siaga Raphael ambapo alisema ajira yake itaanza leo.
“Huyu atafundishwa ufundi wa
kutengeneza vifaa mbalimbali hasa vya watu wenye ulemavu hapa, ili aweze
kusaidia kuwafundisha watu wenye ulemavu wengine.Mradi anataaluma hiyo
ataanza kazi kesho asubuhi (leo asubuhi),”alisema Gupta.
Mkurugenzi Mkuu wa Kamal Steel,
Sameer Gupta, alisema, kampuni hiyo imekuwa mstari wa mbele katika
kusaidia viungo hivyo bandia kwa watu wenye ulemavu ambapo mpaka sasa
imesaidia watu 200.
“Tutaendelea kuwasaidia kila
mara ili tuweze kuisaidiana na serikali yetu kuwaondolea changamoto
wenzetu hawa. Tunaamini wakipewa viungo hivi bandia wanaweza kushiriki
shughuli mbalimbali muhimu zitakazowaingizia kipato,”alisema.
Akizungumza kwa niaba ya wenzake
walio pokea msaada huo, Siaga Raphael, aliipongeza kampuni hiyo kwa
masaada wa vifaa hivyo na kuitaka serikali kuwa kumbuka watu wenye
ulemavu kwa kuwasaidia pia kuwapa taaluma ya ufundi itakazowawezesha
kujimudu kimaisha.