RAIS DK SHEIN ATEMBELEA KAMBI YA KIPINDUPINDU

April 20, 2016

KIP1
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa Daktari dhamana wa Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu Ramadhan Mikidadi Suleiman leo asubuhi alipotembelea kituoni hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja,wengine ni Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo(wa pili kushoto) na naibu Waziri wa Wizara hiyo Harusi Said Suleiman na Katibu Mkuu Dkt.Juma Malik Akili (katikati).[Picha na Ikulu.]
KIP2
Baadahi ya watoa huduma na wananchi wakisubiri huduma katika Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu kama wanavyoonekwanwa wakati Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein alipotembelea kituoni hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja leo asubuhi,[Picha na Ikulu.]
KIP3
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipata maelezo kutoka Mkurugenzi kinga Wizara ya Afya Dk.Mohamed Dahoma (katikati) wakati alipotembelea  Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja leo asubuhi,wengine ni Daktari dhamana wa Kituo cha Maradhi ya KipindupinduRamadhan Mikidadi Suleiman (kushoto)Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya Dkt.Jama Adam Taib(wa pili kushoto),[Picha na Ikulu.]
KIP4
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akitoa maelezo kwa Uongozi wa Wizara ya Afya wakati alipotembelea  Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja leo asubuhi,(wa pili kushoto) Waziri wa Afya Mahmoud Thabiti Kombo, [Picha na Ikulu.]
KIP5
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (kulia) akisalimiana na Mkuu wa Shirika la Kimataifa la LIONS CLUBS Kanda ya Tanzania na Uganda Bw.Hyderall Gangji wakati alipotembelea  Kituo cha Maradhi ya Kipindupindu hapo Chumbuni karakana Wilaya ya Magharibi Unguja leo asubuhi,wengine (kushoto) Mustafa kudrati  LIONS CLUBS Tanzania na Waziri wa Afya Mahmoud Thabit Kombo,[Picha na Ikulu.]
KIP6
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein (katikati) akimsikiliza Mwanamama Siti Akida Makame  mkaazi wa Ziwa Maboga aliyeruhusiwa kurudi nyumbani katika kituo cha Maradhi ya Kipindupindu hapo Chumbuni Karakana Wilaya ya Magharibi Unguja,baada ya kuugua maradhi hayo wakati Rais  alipotembelea  Kituo hicho leo asubuhi,[Picha na Ikulu.]
 

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »