AFRICAN SPORTS KUINGIA KAMBINI JUNI 3.

May 31, 2015
KLABU ya African Sports “Wanakimanumanu”inatarajiwa kuingia kambini Juni 3 mwaka huu kwa ajili ya kujiwinda na Michuano ya Ligi kuu Tanzania Bara msimu ujao baada ya kupanda kucheza daraja hilo.

 Akizungumza jana, Katibu wa timu hiyo, Khatib Enzi aliliambia gazeti hili kuwa wameamua kuingia kambini mapema ili kuhakikisha wanakiandaa vema kikosi chao kwa ajili ya kuhimili mikimiki ya Ligi kuu ikiwemo kupata matokeao mazuri.

Enzi alisema kuwa wachezaji wa timu hiyo waliopo nje ya mkoa wa Tanga kwa sasa watalazimika kutua mkoani hapa Juni Mosi mwaka huu tayari kuungana na wenzao katika kambi yao itakayokuwepo Kata ya Usagara jijini Tanga.

     “Kuanza kambi mapema ni miongoni mwa mipango yetu ya kuhakikisha tunakiandaa kikosi chetu vyema kwani Ligi kuu sio lelemama hivyo inahitajika kujipanga vema “Alisema Enzi.

Katika hatua nyengie,Enzi alisema kuwa usajili ambao wataufanya kabla ya kuanza michuano hiyo utakuwa ni katika nafasi za mlinda mlango, kiungo wa kati na washambualiaji ambao tayari kamati ya usajili ya timu hiyo imeshaanza kazi ya kuhakikisha nafasi hizo zinapata wachezaji makini watakaoiletea maendeleo.

Alisema kuwa msimu ujao wamepania kufanya usajili wa nguvu ambao utawawezesha kurudisha enzi zao za zamani wakati walipopanda daraja na kuchukua ubingwa wa Ligi kuu soka Tanzania bara.

Hata hivyo alisema kuwa klabu hiyo imekwisha kuwafungashia virago wachezaji sita ambao ni Gerary Samburu, Khasim Mkele, Eddy Zaharani, Nyanda Kazioba, Shingwa na Evarist Mujwahuki ambao wapo huru.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »