TANGA UWASA YAANZA MIKAKATI YA KUKABILIANA NA WADAIWA SUGU

March 23, 2015

MAMLAKA ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga (Tanga Uwasa) wameanzisha mipango kabambe ya kukabiliana na wadai sugu kwa kuanza kuwafungia wateja wote mita za luku ambazo zitawalazimu kulipia kabla ya kutumia.

Ambapo mamlaka hiyo inadai kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 1 kwa Taasisi za kiserikali na baadhi kwa makampuni binafasi kitendo ambacho kinapelekea wao kushindwa kufikia malengo yao waliojiwekea ya kukusanya fedha.

 Hayo yalisemwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka hiyo, Salum Shamte wakati wa kilele cha maadhimisho ya wiki ya maji ambapo kimkoa yalifanyika kwenye kata ya Pongwe yaliyoambatana na uzinduzi wa Jengo la watoa huduma la Mamlaka hiyo.

Alisema kuwa hali hiyo itaweza kuisaidia mamlaka hiyo kukusanya fedha za madeni kwa wakati kitendo ambacho kitawawezesha kuweka mipango imara itakayowapa maendeleo ikiwemo kuongeza ufanisi mzuri katika utoaji wa huduma kwa wananchi.
    “Njia hii ya ufungaji wa mita za luku za Maji kwa wateja wetu itatusaidia kupata ufanishi katika ukusanyaji wa mapato yetu hivyo tumeziagiza mita za majaribio ambazo zitaanza kufungwa kwa wale wadaiwa sugu “Alisema Shamte.

Aidha aliwataka watumishi wa mamlaka hiyo wenye tabia ya kushirikiana na wateja kuiba maji kuacha mara moja kwani watakaob ainika hawatavumiliwa watahakikisha wanachukulia hatua kali ili kuweza kukomesha vitendo hivyo.
   “Mtumishi ambaye utabainika kushirikiana na mteja kuiibia mamlaka kwa kuwaunganishia maji kinyemele nakuambia hatutawavumilia lazima tutawachukua hatua kali kwani tusipofanya hivyo tutaendelea kupata hasara “Alisema Shamte.

Kwa upande wake,Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Said Magalula ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kilele hicho alisema kuwa wataendelea kuisaidia mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Jijini Tanga(Tanga Uwasa)ili kuhakikisha inapata fedha zote wanazoodai kwenye Taasisi Sugu ili ziweze kuwasaidia kuendeleza mipango yao.
  “Tutahakikisha ninashirikiana nanyi kuhakikisha wadaiwa sugu wa madeni kwa kuisaidia mamlaka lengo likiwa kuweza kuzipata fedha hizo kwa ajili ya mipango yenu “Alisema RC Magalula.
Hata hivyo alitoa wito kwa wateja wanaodaiwa madeni na mamlaka hiyo kulipa mapema kabla hawajachukuliwa hatua kali.
Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »