Rais
wa TFF, Jamal Malinzi (kushoto) na Mkuu wa Masoko na Mawasiliano wa
Vodacom, Kelvin Twissa wakijiandaa kutiliana saini mikataba yao. Kulia
anayeshuhudia ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi hiyo, Boniface
Wambura.
Malinzi akisistiza jambo kwenye mkutano huo.
Twissa akijibu maswali ya wanahabari hawapo pichani.Mkutano ukiendelea.
KAMPUNI ya
simu za mkononi ya Vodacom leo imetiliana saini na Shirikisho la Mpira
wa Miguu nchini TFF mkataba wa kuendelea kuidhamini Ligi Kuu Tanzania
Bara kwa kipindi kingine cha miaka mitatu. Kampuni hiyo imeendelea
kuidhamini ligi hii baada ya kuidhamini kwa miaka minane mfululizo
iliyopita.
Mkataba huo umetiwa saini
kwenye mkutano na vyombo vya habari uliofanyika Makao Makuu ya Vodacom
yaliyopo Mlimani City Jijini Dar es Salaam.
(PICHA : RICHARD BUKOS / GPL)