DAVID MWAMWAJA: LENGO LETU MSIMU UJAO NI KUIRUDISHA JUU PRISONS

September 04, 2014
Kocha mkuu wa Prisons, David Mwamwaja ( wa kwanza kulia)

Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam,

David Mwamaja hajafanya usajili mkubwa licha ya kikosi chake kupambana hadi dakika ya mwisho msimu uliopita ili kusalia katika ligi kuu.

Baada ya ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Ashanti United, 24 April, Tanzania Prisons ilifanikiwa kubaki katika ligi kuu Bara. Wengi walitaraji timu hiyo ingefanya usajili mkubwa wakati wa dirisha la usajili kwa kuamini kuwa timu hiyo inahitaji mabadiliko makubwa.

 Haijawa hivyo na Mwamaja ameweza kuhakikisha mchezaji wa timu ya Taifa ya Zanzibar, Amir Omary anatua katika kikosi chake kwa lengo la kuongeza makali katika safu ya mashambulizi ambayo ilibebwa zaidi na mshambulizi, Peter Michael na Richard Peter msimu uliopita.

“ Ligi itakuwa ngumu msimu ujao, lakini tunataka kuirudisha juu Tanzania Prisons kama ilivyokuwa enzi za kina Osward Morris.Nimeongezwa katika timu hii kwa lengo la kusaidiana na wachezaji waliopo ili kuifanya Prisons kuwa timu bora msimu ujao.. Tangu nimefika hapa nimepata vitu vingi vipya ndani na nje ya uwanja. Upendo, ushirikiano na umoja ni mambo yaliyotawala hapa” anasema mshambulizi, Amir Omary ambaye amesajiliwa akitokea klabu iliyoshuka daraja ya JKT Oljoro.

Michael alifunga mabao 12 msimu uliopita, Richard alifunga mabao manne na Amir alifunga mabao sita katika kikosi cha Oljoro msimu uliopita na mchexzaji huyo wa Zanzibar Heroes anaamini kuwa umoja wao utawasumbua walinzi wengi msimu wa 2014/15.

“ Ni safu kali ya mashambulizi, kila timu imejiandaa msimu ujao lakini nachoweza kusema tumejipanga kuhakikisha Prisons inafanya vizuri msimu ujao. Mwalimu yoko poa na kila mmoja kikosini anafahamu ni kitu gani ambacho kinatakiwa”

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »