February 04, 2014

MAKAMBA,KINANA NA WENGINE WACHANGIA

          
Raisa Said, lushoto
Zaidi ya Sh. Mil. 41 zimechangwa  kwa  ajili  ya  ujenzi  wa  kanisa katika Chuo  cha Kumbukumbu ya  Sebastian Kolowa (SEKOMU), wilayani Lushoto katika juhudi za kuwasogezea  huduma  karibu wanafunzi  na  jamii  inayozunguka  katika chuo  hicho.

Kwa  mujibu  wa  Makamu  Mkuu wa  Chuo hicho, Dk Aneth  Munga  kati  ya  fedha  hizo, Sh. mil.22  zilichangwa na Mbunge wa Jimbo la Bumbuli, January  Makamba  kwa  kushirikiana  na   baadhi  ya Mawaziri, wabunge  pamoja  na  Katibu  Mkuu wa  CCM, Abdulahman Kinana.

Munga  alisema  kuwa  fedha  zilizochangwa zinawapa  matumaini  makubwa  ya kutimiza  ndoto  ya  ujenzi wa  kanisa  ambao  alisema  ili kukamilika  kwa  ujenzi zinahitajika  Sh. Bil.3.

Dk. Munga  alisema  kuwa  kujenga  si  jambo rahisi na kwamba  michango  walioipata  ni   mwanzo  wa  ujenzi  huo.

Makamu  Mkuu wa  Chuo  huyo alitaja sababu za  kumualika Makamba kuwa ni pamoja na  mchango  wake  katika  shughuli za kijamii na  kujitoa  kuwa  mtetezi  wa  amani. Dr. Munga alisema kuwa mara  nyingi  ameonekana  akisisitiza  juu ya upendo  na  amani kwa  watanzania.

Kwa upande wake, Makamba, ambaye pia ni Naibu  Waziri  wa  Mawasiliano  Sayansi alisema  kujengwa  kwa  kanisa  hilo ni  chachu  katika  jamii ya  wanafunzi  walioko chuoni  hapo  pamoja  na  wananchi  waishio  maeneo  ya  jirani.

Pia alisisitiza juu ya  umuhimu wa kudumisha  amani  na  upendo  uliopo  ili  Baraka  za  Mwenyezi  Mungu

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »