NAKUMBUKA bao ambalo
nililifunga wakati nimesajiliwa na Yanga liliweka rekodi ya kufuta uteja wa
timu hiyo kwa wapinzani wao Simba kwa kipindi cha miaka saba iliyopita kwa
kufunga bao na hivyo kupelekea shangwe na nderemo katika mitaa ya Jangwani.
Kauli hii aliitoa
mshambuliaji wa zamani wa Yanga,Benard Mwalala ambaye kwa sasa ni kocha mkuu wa
timu ya Halmashauri FC ya Muheza anasema baada ya kufunga bao hilo alishangaa
kuona uwanja mzima ukilipuka kwa kelele kitendo ambacho kilimfanya kuhisi
upinzani wa timu hizo mbili ni mkubwa sana.
Akizungumzia histori yake
binafsi kuhusu maisha ya soka ,Mwalala anasema alianza kucheza mpira ya miguu
mwaka 2000 akiwa na timu ya Nzoia Sugar ya Kenya
ambapo aliichezea kwa kipindi cha miaka mitatu na kuhamia timu ya Villa SC ya Uganda
kuanzia mwaka 2003 mpaka 2006.
Anasema baada ya kumaliza
mkataba wake na Villa SC
ya Uganda aliamua kuja
nchini Tanzania kujiunga na
Mabingwa wa Ligi kuu Tanzania
bara Yanga mwaka 2006 ambapo aliweza kudumu na timu hiyo kwa kipindi cha miaka
miwili.
Mwalala anasema mwaka 2009
aliamua kuondoka hapa nchini kuelekea nchini Malaysia kujiunga na timu ya PDRM
ambapo alifanikiwa kuichezea kwa kipindi cha mwaka mmoja kabla ya kurejea Yanga
mwaka 2010 kuendeleza harakati zake za kisoka.
Kama unavyojua maisha ya
mpira ya miguu ni kutafuta maslahi mwaka huo huo,Mwalala aliiacha timu hiyo na
kutimkia nchini Omani kujiunga na timu ya Sur ambapo aliingia mkataba wa mwaka
mmoja na baada ya hapo akarejea nchini kujiunga na mabingwa wa soka Tanzania bara 1988 Coastal Union
“Wagosi wa Kaya”
Anaeleza kuwa aliweza
kuichezea Coastal Union ya Tanga kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2011 mpaka 2012
alipoamua ondoka kwa kukosa nafasi ya kuichezea baada ya kumalizika msimu wa
ligi kuu Tanzania
bara.
Baada ya kuondoka kuacha kucheza Coastal Union,Mwalala
alikwenda kusomea mafunzo ya Ukocha wa mpira wa miguu na kupata mafunzo hayo
ngazi ya juu kutokana na umahiri wake na kupenda kazi yake aliweza kupata timu
ya soka Halmashauri FC ya Muheza inayoshiriki Ligi ya Mkoa wa Tanga.
Akizungumzia sababu zilizompelekea yeye kupenda kuwa mwalimu
wa mpira wa miguu,Mwalala anasema kilichomvutia ni kutokana na majukumu
aliyowahi kupewa wakati akichezea Coastal Union ambapo yeye alikabidhiwa jukumu
la kuifundisha timu hiyo wakati Kocha wao Mkuu,Jamhuri Kiwelu alipokwenda Dubai
kusoma.
Anaeleza kuwa alipoachiwa jukumu hilo
aliweza kuwaongoza vema wachezaji wenzake kwa kipindi cha mwezi mmoja na nusu
kwa mafanikio makubwa yaliyopelekea wao kufanya vizuri katika michezo yao ya Ligi kuu iliyokuwa
ikifuatia kabla ya Juma Mgunda kukabidhiwa kuinoa timu hiyo.
Mwalala anaeleza kuwa wakati akiwa mchezaji alianza
kushughulika na masuala ya ukocha mpaka alipoamua kutundika daluga rasmi mwaka
2011 na kuingia rasmi kwenye mafunzo ya ualimu wa mpira wa miguu.
Anasema kitu ambacho hatoweza kukisahau maishani kwake
kuhusiana na soka ni wakati alipokuwa akichezea Yanga alikwenda mazoezini akiwa
amevalia jezi ya Kenya ambayo ni nyekundu kitendo
ambacho kiliwauzi mashabiki wa Yanga.
Mwandishi wa Makala hii alimuuliza Mwalala anadhani nini
kifanyike Tanzania ili soka
letu liweze kupiga hatua kubwa kama zilivyo nchi nyengine duniani,Mwalala
anasema Tanzania inabahati
kubwa sana kwa
kuwa watanzania wanapenda mpira lakini miongoni mwao waache siasa ili kuweza
kupata mafanikio.
Anaongeza kuwa lazima ufike wakati wachezaji wakubaliana kwa
kauli moja kwenda kutafuta maisha ya mpira nchi za nje ili kuweza kuwapa nafasi
wachezaji chipukizi nao waweze kuonekane pamoja na kuwa na utamaduni wa kucheza
la nje ili kuleta ushindani wao kwa wao.
Aidha analitaka shirikisho la soka hapa nchini (TFF)kuhakikisha
linaweka mkakati wa kuwalinda wachezaji kwa sababu kuna mikataba mingi ya
wachezaji inavunjwa bila kufuatwa kwa utaratibu bila wao kuingilia kati lengo
likiwa kuweza kuwapa motisha bila kuwepo upendeleo wa aina yoyote ile.
Halikadhalika aliushauri uongozi mpya wa shirikisho la soka
ulioingia madarakani chini ya Rais wake,Jamali Malinzi kuhakikisha wanaongeza
idadi ya timu zinazoshiriki Ligi kuu Tanzania bara ili viweze kuwa zaidi
ya kumi na nne vilivyopo hivi sasa kwa sababu hakuna mashindano mengine ya
kuchezwa zaidi ya hayo.
Mwalala pia anatoa ushauri kwa vilabu vyote vinavyoshiriki
Ligi kuu kuhakikisha wanaziingia kwenye mashindano mbalimbali timu zao B kabla
ya timu kubwa kucheza au kuingizwa kwenye ligi za wilaya ya mikoa ili kuwa kuwa
na wachezaji wazuri imara na ambao
wataleta ushindani.
Mshambuliaji huyo wa zamani hakusita kuzungumzia suala la
shirikisho hilo kuwatafuta wadhamini kwa ligi
daraja la kwanza na ligi kuu soka Tanzania bara hasa kwa vikosi vya B
ili kuweza kuleta mabadiliko makubwa katika soka letu na Taifa kwa ujumla
Akizungumza suala la viwanja vya soka hapa nchini,Mwalala
aliishauri Serikali kupitia wizara ya michezo na utamaduni kuhakikisha
inalisimamia suala hilo
kwa kuweka msukumu mkubwa kwa viwanja ili kuwawezesha vijana kushiriki michezo
kikamilifu.
Mwisho.
Mwandishi wa Makala hii anapatikana kupitia
anapatikana kupitia 0714543839/0754000186.