MAZIBA : “Makamu Mwenyekiti mpya Halmashauri ya wilaya ya Mkinga”

June 29, 2013

Na Oscar Assenga, Mkinga.
DIWANI wa Kata ya Mkinga (CCM), Juma Maziba amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Mkinga kwa kipindi chengine mara baada ya kumshinda mpinzani wake Nassoro Mbaruku wa (CUF) kwenye uchaguzi uliofanyika juzi kutokana na Makamu huyo kumaliza muda wake kikatiba.

Akitangaza matokeo hayo Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo, Cheyo Nkelenge alimtangaza Juma Maziba kuwa mshindi katika nafasi hiyo baada ya kupata uwa 19 dhidi ya mpinzani wake aliyepata kuwa 9 katika uchaguzi huo kati ya kura 28 zilizopigwa na wajumbe.

Baada ya kutangazwa matokeo hayo, Maziba aliwashukuru wajumbe waliomuwezesha kuchaguliwa kwa mara nyengine tena na kuhaidi kuwa mstari wa mbele kumshauri mwenyekiti wa halmashauri masuala ya kimaendeleo katika wilaya hiyo kama ilivyokuwa katika awamu yake iliyomalizika.

Alisema ushindi ambao ameupata umempa faraja kuona jinsi gani anavyokubalika na madiwani wenzake na kuhaidi kuendeleza ushirikiano kwenye shughuli zao ili kuweza kuchochoa kasi ya maendeleo kwa wananchi wao.

(Picha kushoto ni Makamu Mwenyekiti huyo alipeana mkono na mpinzani wake diwani wa kata ya Moa)

Makamu huyo alichaguliwa katika nafasi hiyo katika kipindi cha        mwaka 2010-2013 kabla ya kuchaguliwa tena kushika wazifa huo ambapo amesema matarajio yake makubwa ni kushirikiana na viongozi wenzake ili kusukuma kasi ya maendeleo kwenye maeneo yao.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »