Mwenyekiti Halmashauri awaasa watumishi wa serikali.

June 29, 2013

Na Oscar Assenga, Mkinga.
MWENYEKITI wa Halmashauri ya wilaya ya Mkinga,Andrew Ngoda amewataka watumishi wa halmashauri kuepuka kusukumwa na itikadi na hisia zao za kisiasa ,dini,kabila na maeneo yao katika kutekeleza majukumu yao kwani wanawajibika,kufuatilia na kuratibu utekelezaji wa maamuzi ya halmashauri kwa kuzingatia mtiririko wa uongozi.

Ngoda ametoa kauli hiyo leo wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani ambacho kilikuwa kwa ajili ya madiwani kuwasilisha taarifa za miradi ya maendeleo kwenye kata zao kabla ya kufanyika kikao kingine kesho.

Mwenyekiti huyo amesema maadili yanaweza kuwasukuma madiwani kuheshimu nafasi na hadhi madiwani wenzao hali kadhalika watumishi wa halmashauri wazingatie kwa kiwango cha juu uadilifu kwa kuzingatia sheria, kanunu na miongozo ya utawala bora katika utendaji wao.

Ameongeza kuwa watumishi wa ngazi zote baadhi wanaanguka sana kwenye uwazi na uwajibikaji ambapo amewataka kuelewa kuwa uwazi ni kufanya jambo bila kificho na uwajibikaji ni kuwasilisha taarifa ya dhamana ya utendaji wao kwa aliyekupa dhamana.

Aidha amewaeleza kuwa uwajibikaji ni msingi wa utawala bora ambao unawataka watumishi katika ofisi za umma kuwajibika kwa matendo yao ili kuleta imani kwa wananchi wanaowaongoza katika maeneo husika.

Ameeleza kuwa uwazi unawezesha uelewa na ufuatiliaji wa mchakato ili kujua kama unaendeshwa kwa kuzingatia misingi ya sheria na kanuni zake na kufikia malengo yaliyotarajiwa kufikiwa na kueleza uwajibikaji,uwazi vyote viwili ni muhimu katika kusaidia matumizi sahihi bora kwenye kuendesha masuala ya halmashauri na nchi katika ngazi zote.

Hata hivyo amesisitiza utawala bora kwenye maeneo yote uzingatiwe hivyo kwa vile fedha zinapatia kwenye kitengo cha manunuzi ambapo amewataka kuzingatia mpiango sahihi, nyaraka sahih, kuwahi katika kuitisha zabuni, ufanisi na kutenda haki na kutenda haki katika mchakato wa tathimini za zabuni.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »