NYUMBA 12 ZA WAVAMIZI WAHIFADHI YA MISITU ZATAKETEZWA KWA MOTO PANGANI

June 29, 2013


Na Amina Omari,Pangani
Jumla ya Nyumba 12 zilizokuwa zimejengwa na wahamiaji haramu jamii ya wafugaji  ndani ya hifadhi ya msitu wa Msububwe wilayani Pangani Mkoani Tanga zimeteketezwa kwa moto na kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo ikiwa ni katika oparesheni ya kuondosha wavamizi wa hifadhi hiyo .
Zoezi hilo ambalo linalenga kulinga hifadhi ya msitu huo dhidi ya wavamizi hao wa  kabila la wamang”ati ambao walikuwa wamevamia hifadhi na kuanza kufanya uharibu wa kuharibu  vyanzo vya maji,  kukata miti hovyo ya kujengea nyumba , kuni pamoja na kuchunga mifugo yao.

Akiongea na gazeti hili wakati wa oparesheni hiyo Kaimu Katibu Tawala wa Wilaya hiyo Pilika Kasanda alisema zoezi hilo litakalo dumu kwa muda wa siku tano  la kuwamisha na kuharibu makazi ya wavamizi hao ili kulinga  hifadhi hiyo isiendelee kuharibiwa.

“Zoezi hili limeanza leo na litadumu kwa siku tano katika kukagua na kuwaondosha kwa nguvu wavamizi wote wafugaji walioko ndani ya hifadhii kwani wameanza uharibu wa vyanzo vya maji ambavyo ndio tegemeo pekee la wilaya hii”alisema Kasanda.

Alisema  wafugaji ho wamekuwa wakivamia msitu huo mara kwa mara licha ya juhudi mbalimbali walizozichukuwa za kuwapa elimu kuhusu umuhimu wa hifadhi hiyo na kuwataka warudi katika makazi yao ya awali lakini imeshindikana.

Hata hivyo Meneja hifadhi msitu huo John Mkenda alisema kabla ya zoezi hilo walianza kutoa elimu kwa jamii  inayozunguka hifadhi kuhusu umuhimu wa hifadhi hiyo na madhara ya uharibufu unaofanyika ili kuhakikisha wanalinda hifadhi na viumbe vilivyoko.

“Tulianza kutembelea vijiji vinavyozunguka hifadhi ili kutoa elimu ya mazingira kisha tukawatembelea na wavamizi ambao ni jamii ya wamasai na kuwashauri watoke kwa amani kabla ya hatua za kisheria kuanza kufuatwa ,tunashukuru walitii ili wengine walikaidi”alisema Mkenda.

Aliongeza kuwa nyumba nne hawakuzichoma moto kutoka na kutowakuwa wazazi bali wapo watoto pekee lakini nao wamewapa siku mbili kuondoka kwa hiari kabla ya kuanza kuchoma moto nyumba hizo pamoja na vitu vyao.
MWISHO

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »