WIZARA ya Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo yapewa changamoto.

June 29, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.

SERIKALI kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo imeshauriwa kuweka utaratibu wa kukaa na makocha wa kigeni wanaofundisha timu za Taifa muda mrefu ili kuweza kupata mafanikio badala ya kuwabadilisha kila wakati kitendo ambacho kinadumaza soka badala ya kupiga hatua kwenda mbele.



Ushauri huo ulitolewa na Golikipa wa zamani wa timu ya Coastal Union ya Tanga, Nyendi Mpangala wakati akizungumza na mwandishi wa blog hii hivi karibuni ambapo alisema kitendo cha ubadilishwaji wa makocha hao kunawafanya hata wachezaji wenyewe kutokuelewa kile wanachofundishwa kutokana na kila kocha mpya anakuwa na mbinu zake.



Nyendi aliwahi kuichezea Costal Union ya Tanga kati ya mwaka 2000-2003 alipoamua kuacha kujishughulisha na mambo ya soka hapa nchini na kueleza mpira wa sasa hivi ni tofauti na zamani kutokana na enzi hizo wachezaji wengi walikuwa na vipaji vyao binafsi kuliko ilivyokuwa wakati huu .



Alisema ili soka letu hapa nchini liweze kupiga hatua ni lazima serikali ihakikishe wanahamasisha wadau kuanzisha vituo vya mafunzo ya soka (Academy) ambazo zitakuwa imara kwa ajili ya maendeleo ya soka hapa nchini ikiwemo kuvilinda vipaji hivyo pamoja na kulinda viwanja vya michezo vilivyopo maeneno mbalimbali na kuwapa fuksa wachezaji kucheza.



Akizungumzia nafasi ya mlinda mlango alisema ni ngumu lakini ni rahisi endapo wachezaji wenyewe wataipenda kutokana na kuwa nafasi ambayo mara moja unaweza kupata nafasi ya kwenda kucheza kwenye timu nyengine ikiwemo timu ya Taifa kwa sababu ni mahali ambapo mtu anaonekana.



Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »