Ufinyu wa bajeti kikwazo PSPF Tanga.

June 29, 2013

Na Oscar Assenga, Tanga.
UFINYU wa Bajeti wa maeneo salama ya uwekezaji ambayo yatahakikisha urejeshaji wa mtaji na kupata faida kwa wakati uliokusudiwa ni miongoni mwa changamoto ambazo zinaukabili mfuko wa Pensheni kwa watumishi wa Umma PSPF mkoa wa Tanga.

Meneja wa Mfuko huo Mkoani hapa, Salome Makalla aliyasema hayo wakati akitoa Mada kwa wafanyakazi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tanga hivi karibuni ambapo alisema changamoto nyengine ambayo wanayokabiliana nayo ni ongezeko la mfumuko wa bei unaosababisha kukosekana kwa faida hali na hivyo kuathiri thamani ya fedha iliyowekezwa.

Makalla alisema kuwa suala lengine ambalo limekuwa kikwazo kikubwa kwao ni kukosekana kwa nyaraka muhimu wakati wa kuomba mafao imekuwa ikiathiri wastaafu kwakuwa mapungufu hayo husababishwa kuchelewa kwa malipo na hivyo kushindwa kumudu mahitaji ya kila siku baada ya ustaafu kazi.

Alisema licha ya kumuathiri mstaafu pia mfuko umekuwa ukiathirika kwa kushindwa kutimiza lengo lake la kulipa mafao kwa wakati.

Aidha alisema mikaati yao ya baadae ni kuviwezesha vikundi vya kuweka aiba na kukopa Saccos vya wanachama ambapo mfuko unafanya tathimini ya namna bora ya kuviwezesha vikundi hivyo kujiendesha na kukopesha wanachama wake zaidi kwa wingi.

Aliongeza kuwa mfuko unatarajia kuwa unavikopesha vikundi hivyo kwa riba nafuu ili viweze kuwapatia mikopo ya kujiendeleza wanachama wao ambapo pia ni wanachama wa mfuko wa PSPF.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »