MABAO 191 na Kadi 163 zapatikana ligi ya wilaya ya Tanga.

March 08, 2013

Na Mwandishi Wetu,Tanga.
Katika hatua ya mchujo ya Ligi wilaya ya Tanga iliyoanza mwishoni mwa mwezi septemba mwaka jana na kumalizika Januari 6 mwaka huu jumla ya mabao 191 yalifungwa na timu zilizokuwa zikishiriki ligi hiyo.

Katibu Msaidizi wa Chama cha soka wilaya ya Tanga (TDFA) Salim Carlos alisema kuwa mabao hayo yalitokana na michezo 64 iliyochezwa kwenye hatua hiyo ambayo ilikuwa ikishirikisha timu 41 ambazo zilikuwa zimegawanywa kwenye makundi kumi.

Carlos alisema baada ya kumalizika hatua hiyo kila kundi tiyari limekwisha kutoa washindi wawili ambao wanaendelea na ligi hiyo katika msimu mpya wa mwaka 2012-2013.

Alisema pia katika hatua hiyo jumla ya kadi zipatazo163 ambapo kati ya hizo kadi za njano zilikuwa ni 143 wakati kadi nyekundu zilikuwa 20 na  timu iliyoongoza kupewa kadi nyingi za njano ni Raidon ambapo timu hiyo ilipewa kadi 8.

Aidha alisema katika hatua hiyo wachezaji Hussein Salim wa timu ya Donge Fc Rubein Desideri na wa Younga Rovers waliongoza kwa kufunga mabao ambapo kila mmoja alifunga mabao 15.

Akizungumzia changamoto ambazo zilijiotokeza katika hatua hiyo, Katibu huyo alisema uhaba wa fedha za uendeshaji ni moja kati ya vitu ambavyo vilijitokeza hali iliyopelekea kushindwa kuwalipa waamuzi na pesa za kulipia uwanja kwa wakati.

Katibu huyo aliwataka wadau mbalimbali wa soka mkoani hapa kukisaidia chama hicho ili kiweze kufanikisha ligi yao msimu huu kwani wamedhamiria kuinua kiwango cha soka wilayani hapa.

Mwisho.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »