Na Mwandishi Wetu,Tanga.
Katika hatua ya mchujo ya Ligi wilaya ya Tanga iliyoanza mwishoni mwa mwezi
septemba mwaka jana na kumalizika Januari 6 mwaka huu jumla ya mabao 191
yalifungwa na timu zilizokuwa zikishiriki ligi hiyo.
Katibu Msaidizi wa Chama cha soka wilaya ya Tanga (TDFA) Salim Carlos
alisema kuwa mabao hayo yalitokana na michezo 64 iliyochezwa kwenye hatua hiyo
ambayo ilikuwa ikishirikisha timu 41 ambazo zilikuwa zimegawanywa kwenye
makundi kumi.
Carlos alisema baada ya kumalizika hatua hiyo kila kundi tiyari limekwisha
kutoa washindi wawili ambao wanaendelea na ligi hiyo katika msimu mpya wa mwaka
2012-2013.
Alisema pia katika hatua hiyo jumla ya kadi zipatazo163 ambapo kati ya hizo
kadi za njano zilikuwa ni 143 wakati kadi nyekundu zilikuwa 20 na timu iliyoongoza kupewa kadi nyingi za njano
ni Raidon ambapo timu hiyo ilipewa kadi 8.
Aidha alisema katika hatua hiyo wachezaji Hussein Salim wa timu ya Donge Fc
Rubein Desideri na wa Younga Rovers waliongoza kwa kufunga mabao ambapo kila
mmoja alifunga mabao 15.
Akizungumzia changamoto ambazo zilijiotokeza katika hatua hiyo, Katibu huyo
alisema uhaba wa fedha za uendeshaji ni moja kati ya vitu ambavyo vilijitokeza
hali iliyopelekea kushindwa kuwalipa waamuzi na pesa za kulipia uwanja kwa
wakati.
Katibu huyo aliwataka wadau mbalimbali wa soka mkoani hapa kukisaidia chama
hicho ili kiweze kufanikisha ligi yao
msimu huu kwani wamedhamiria kuinua kiwango cha soka wilayani hapa.
Mwisho.
|
Next
« Prev Post
« Prev Post
Previous
Next Post »
Next Post »