Na Mwandishi Wetu, Tanga.
JUMLA ya timu 13 zimefunzu kucheza Ligi ya Mkoa wa Tanga mzunguko wa pili
baada ya kufanya vizuri mzunguko wa kwanza na itachezwa kwa mfumo wa nyumbani
na ugenini.
Akizungumza na Blogi hii Katibu wa chama cha soka Mkoa wa Tanga (TRFA), Beatrice
Mgaya alisema maandalizi ya hatua hiyo yamekamilika na mzunguko huo utaanza
Machi 9 mwaka huu.
Mgaya alisema katika ufunguzi wa mzunguko huo, timu za soka Lushoto
Shooting na Korogwe United zinatarajiwa kuonyeshana kazi katika uwanja wa soka
Lushoto na unatarajiwa kuwa na upinzani mkubwa.
Alisema mchezo mwengine utakaochezwa siku hiyo utafanyika
kwenye uwanja wa Mkwakwani ambapo timu ya maafande wa jeshi la magereza
mkoani hapa Small
Prison watakapoikabili Viva Dynamo ya Maramba wilayani Mkinga.
Katibu huyo alizitaka timu zinazoshiriki ligi hiyo kuonyesha nidhamu ya
hali ya juu ili kuweza kuleta ushindani pamoja na kuziasa zifanye maandalizi ya
kutosha kabla ya mechi zao.
Mgaya alizitaja timu zinazoshiriki kuwa ni Lushoto Shooting, Korogwe
United,Halmashauri Fc,Lushoto Star,Small Prison,Viva Dynamo, ,Veteran FC,Monga
Star,African Sports,Black Burn,Eagle Rangers na Moa Original na Makorora Star.
Timu hizo zitachukuana ili kuweza
kupatikana bingwa wa mkoa katika msimu huu ambapo ataweza kushiriki mashindano
ya mabingwa wa mikoa itakayochezwa baada ya kumalizika ligi za mikoa.
Mwisho.
Na Mwandishi Wetu,Handeni
LIGI ya soka kuwania kombe la Diwani kata ya Kwamgwe wilayani hapa,juzi ilifikia tamati kwa mchezo kati ya Bondo United na Mungano FC ambapo matokeo ya mchezo huo Bondo ilitwaa ubingwa kwa njia ya penati kwa kuwanyuka wapinzani wao kwa 3 - 0.
Katika mchezo huo wa fainali uliofanyika uwanja wa Kwedigongo hadi muda wa kawaida unamaizika hakuna mbabe ambapo mwamuzi wa mchezo huo Mohamed Chombo aliongeza muda wa nyongeza dk 15 ambazo pia hazikutoa mshindi hadi hatua ya penati.
Waliofanikiwa kuzikwamisha wavuni penati za Bondo ni Charles Ernest,Hemed Athumani na Hamisi Mohamed wakati ile ya Muungano ilifungwa na mchezaji Enock Juma matokeo ambayo yaliifanya Bondo United kuwa bingwa baada ya penati tano tano kupigwa.
Bingwa wa ligi hiyo ambayo hufanyika kila mwaka aliweza kuzawadiwa kikombe,jezi seti moja na Tsh 100,000, wakati mshindi wa pili timu ya Muungano ilizawadiwa Tsh 70,000 na mshindi wa tatu Tsh 50,000 ambazo zilikwenda jkwa klabu ya soka ya Mbogoni FC.
Mratibu wa mashindano hayo ambaye ni diwani wa kata ya Kwamgwe Sharrifa Abebe akizungumza baada ya mchezo huo kumalizika alisema,amefurahishwa na wachezaji pamoja na mashabiki wa timu zilizoshiriki kuzingatia suala la nidhamu mchezoni.
Alisema mashindano hayo yameweza kutoa timu ya kata ainayoundwa na wachezaji wapatao 40 ambao watakuwa chini ya mwalimu wao msaidizi aliyemtaja kwa jina la Hamza Manulanula huku jitihada za kumtafuta kocha mkuu zikiendelea kufanywa.
"Nimefurahi ligi kumalizika kwa amani na sasa tunaangalia suala la timu yetu ya kata,mwalimu msaidizi amepatikana...mimi na wafadhili wengine tunasaka kocha mkuu ili kuwanoa vyema vijana wetu,tutakuwa na mechi nyingi za majaribio"alisema Sharrifa.
Alisema,lengo la kuanzishwa ligi hiyo ni kukuza vipaji sanjari na kutengeneza ajira kwa vijana huku akibainisha kuwa kupitia ichezi pia vijana itawasaidia kuepukana na mazingira ambayo yanaweza kuwatumbukiza katika vitendo hatarishi na kuharibu maisha yao.
Mwisho.
EmoticonEmoticon