MBARAWA AMKABIDHI NAIBU SPIKA MWONGOZO WA WATUMIAJI WA HUDUMA NA BIDHAA ZA MAWASILIANO

February 08, 2018
  Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson akionesha Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa kwa niaba ya Wabunge. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma Februari 8, 2018.

  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa pili kushoto) akimkabidhi Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson  (wa pili kulia) Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano kwa niaba ya Wabunge. Wakishuhudia  watatu kushoto ni Naibu Katibu Mkuu wa Mawasiliano Mhandisi Anjelina Madete na wa pili kulia ni Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma Februari 8, 2018.

  Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa kwanza kushoto) akimweleza Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson  (wa kwanza kulia) umuhimu wa Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano kwa Wabunge mara baada ya kumkabidhi Mwongozo huo kwa niaba ya Wabunge ili waweze kusoma, kuelewa na kuelimisha wananchi namna ya kutumia vema huduma na bidhaa za mawasiliano nchini. Mazungumzo hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma.

  Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Mhandisi James Kilaba (wa kwanza kushoto) akifafanua jambo kwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson  (wa kwanza kulia) kuhusu Mwongozo wa watumiaji wa huduma na bidhaa za mawasiliano mara baada ya kukabidhiwa na Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa kwa niaba ya Wabunge. Makabidhiano hayo yamefanyika ofisini kwa Naibu Spika, Bungeni mjini Dodoma

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »