VIDEO – MZEE ALIYEGUNDUA NA KUOKOA KUTEKETEA KWA MAKAA YA MAWE MGODI WA NGAKA AOMBA KUKUTANA NA RAIS

April 11, 2018



Mzee Benedict Mapunda (Rasha) mwenye umri wa miaka 66 mkazi wa kijiji cha Ntunduwaro ndiye aliyegundua kuteketea kwa moto kwa mgodi wa madini ya makaa ya mawe Ngaka uliopo Wilaya ya Mbinga Mkoa wa Ruvuma mwaka 2006.

Mgodi huo hivi sasa unaingiza mabilioni ya fedha kwa Kampuni binafsi ya uchimbaji wa madini hayo ya TANCOAL na serikali inalipwa kodi na ushuru kutokana na kazi ya uchimbaji na usafirishaji wa madini hayo ilioanza tangu mwaka 2011.

Mzee Rasha bado hajatambulika kwa kuokoa rasilimali adimu ya madini ya makaa ya mawe kwa nchi yake ambayo yalikuwa yanateketea kwa moto ardhini kwa miaka kadhaa. Rasha anafanyakazi ambayo haifanani na umri wake katika Kampuni ya TANCOAL kwenye mgodi wa Ngaka.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »