Naibu
Waziri Mhe. Injinia Stella Manyanya afungua rasmi mkutano kwa njia ya
Mtandao yaan (Video Conference) wa Wizara ya Viwanda, Biashara na
Uwekezaji na Mamlaka za mikoa na Halmashsauri za Wilaya kuhusu masuala
ya sekta ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji pamoja na taasisi zake leo
Tarehe 18 – 20 Disemba, 2017 na kuunganisha wadau kutoka mikoa ya Mbeya,
Songwe, Kilimanjaro, Ruvuma, Kigoma, Lindi, Singida, Pwani na Dodoma.
Mhe.
Naibu Waziri aliwashukuru Makatibu Tawala wa Mikoa, Wasaidizi wao na
Wakurugenzi wa Halmashauri za wilaya ambao wameitikia wito pamoja na
wataalamu na maafisa mbalimbali.
Wizara
ilianza na taasisi yake ya BRELA ambayo ilielezea majukujumu yake na
huduma mbalimbali wanazotoa kwa umma na kutoa fursa ya wadau kutoka
mikoa yote iliyoshiriki walipata fursa ya kuuliza maswali na kujibiwa
papo kwa papo.