MH. MWAKYEMBE ASHUHUDIA MV. RUVUMA IKIINGIZWA ZIWA NYASA KWA MAJARIBIO

March 02, 2017
unnamed
Mhe. Dkt Harrison Mwakyembe, Waziri wa Mambo ya Katiba na Sheria na Mbunge wa Kyela , ameshudia zoezi la kuingizwa majini kwa Meli mpya ya pili ya mizigo iitwayo MV Ruvuma kwenye bandari ya Itungi, Wilayani Kyela. 
Tukio hilo la kuiingiza Meli hiyo making limefanyika Machi Mosi . Meli hiyo yenye uwezo wa kubeba mzigo zaidi ya tani 1000 inaungana na Meli nyingine mpya MV Njombe yenye uwezo wa kubeba zaidi ya tani 1000 ambayo iliingizwa majini siku tano zilizopita. Meli zote mbili zipo kwenye hatua ya mwisho ya utengenezaji na majaribio kabla hazijaanza rasmi kubeba mizigo kwenye ziwa Nyasa. 
Tayari wateja mbalimbali wamejitokeza kutaka mizigo yao ianze kubebwa yakiwemo makampuni yanayojishughulisha na biashara ya makaa ya mawe.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »