SERIKALI YA MOROCCO KUWEKEZA KATIKA KUKABILIANA NA ATHARI ZA MABADILIKO YA TABIANCHI.

April 07, 2017
SS
Kulia Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina katika Mazungumzo kuhusina na suala la NIshati ya jua na Balozi wa Morocco Nchini Mhe. Benryane Abdelilah (katikati) kushoto ni Msaidizi wa Balozi Bw. Mrabet Yazane.
SS 1
Katikati Balozi wa Morocco Nchini Mhe. Benryane Abdelilah akimsalimia Naibu Waziri ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, alipomtembelea Ofisini kwake, Kulia ni Msaidi wa Balozi Bw. Mrabet Yazane.
SS 3
Kulia Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina akipena Mkono na Balozi wa Morocco nchini  Mhe. Benryane Abdelilah alipomtembelea ofisini kwake Mtaa wa Luthuli jijini Dar es Salaam leo.
SS 2
Kulia msaidizi wa Balozi wa Morocco Bw. . Mrabet Yazane akimsalimia Naibu Waziri Mpina, kulia kwake ni Mhe Balozi . Benryane Abdelilah. (Picha na Evelyn Mkokoi wa OMR)
……………
NA ; Evelyn Mkokoi Dar es Salaam
Serikali ya Morocco iko tayari kushirikiana na Tanzania katika suala zima la kukabiliana na athari zitokanano na mabadiliko ya tabianchi kwa kuwekeza kati mradi mkubwa wa Nishati ya jua.
Akizungumza na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Mhe. Luhaga Mpina Ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, Balozi wa Serikali ya Kifame ya Morocco Mhe. Benryane   Abdelilah  amesema kuwa, Morocco ipo tayari kuwekeza katika mradi mkubwa wa nishati ya Jua yani Solar energy, ili kuweza kusaidiana na Tanzania katika suala zima la kukabiliana na athari zitokanazo na mabadiliko ya tabia nchi, kuongeza kipato katika sekta mbali mbali pamoja na kupunguza uzalishaji wa gas joto.
Pamoja na hilo, Balozi Abdelilah ameitaka idara, kuainisha maeneo ya vipau mbele kwa upande wa mazingira na kusema  kuwa, mradi huo mkubwa wa uzalishaji wa  Nishati ya jua utakaotekelezwa na kampuni kutoka Morocco ya Masen Campany Limited, utasaidia kuongeza matumizi ya nishati mbadala, pamoja na kujenga mahusiano mazuri baina ya nchi hizi mbili hasa katika sekta husika.
Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi hya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina, alisema kabla ya uwekezaji wa mradi mkubwa wa aina hiyo, inatakiwa kufanyika kwa tathmini ya athari ya mazingira na kumuahaidi balozi kuwa watakapokuwa tayari zoezi hilo litafanyika kwa haraka , kwani uwekezaji huo utasaidia kupunguza kwa kiasi kikubwa uharibifu wa mazingira utokanao na ukataji wa miti kwa matumizi ya nishati ya kupikia na mradi utawafikia wananchi wengi walio mbali na gridi ya taifa.
“kutokana na kukauka kwa vyanzo vingi vya maji kunakosababishwa na athari za mabadiliko ya tabianchi, mradi huu utakuwa mbadala wa tatizo hilo, huu ni mradi ambao utatusaidia, Alisisitiza Mpina.”
Balozi wa Morocco Mhe. Benryane Abdelilah alimtembelea Naibu Mpina Ofisini kwake Mtaa wa Luthuli Jijini Dar es Saalam ikiwa ni katika kufahamiana katika utendaji baada ya kufunguliwa kwa Balozi hiyo Nchini.

Share this

Related Posts

Previous
Next Post »