Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisaini Kitabu cha
Maombolezo ya msiba wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Marehemu,
Pascal Mabiti, wakati wa shughuli ya Msiba iliyofanyika nyumbani kwa
marehemu, Upanga jijini Dar es Salaam, leo Okt. 15, 2015.
Picha na OMR
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwafariji
wanafamilia wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Marehemu Pascal Mabiti, wakati wa
shughuli ya kuaga mwili wa marehemu iliyofanyika nyumbani kwa marehemu
Upanga jijini Dar es Salaam, leo Okt. 15, 2015.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akitoa heshima za
mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu marehemu,
Pascal Mabiti, wakati wa shughuli za kuaga zilizofanyika nyumbani kwa
marehemu, Upanga jijini Dar es Salaam, leo Okt. 15, 2015.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, akitoa
heshima za mwisho mbele ya Jeneza lenye mwili wa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu
marehemu, Pascal Mabiti, wakati wa shughuli za kuaga zilizofanyika
nyumbani kwa marehemu, Upanga jijini Dar es Salaam, leo Okt. 15, 2015.